Sunday, December 23, 2012

JE NI WAKATI GANI WA KUNUNUA HISA WENYE MANUFAA ZAIDI KWA MWEKEZAJI?

Kwa Mwanahisa kujua hasa ni wakati gani wa kununua hisa, hiyo tayari ni sehemu ya uwekezaji katika Soko la hisa la Dar es salaakm. Lakini wawekezaji wengi wa ndani hawaoni fursa hii kwa kukosa au kutokuwa na taarifa/maarifa muhimu kuhusu uwekezaji kwenye hisa. Moja ya wakati mzuri wa kuwekeza kwenye hisa ni pale ambapo kampuni inato hisa zake sokoni ili kuongheza mtaji wake (Initial Public Offers - IPO), wakati huo hisa huuzwa kwa bei ya chini na baada ya daftari la hisa kufungwa na kupelekwa kenye soko la hisa la Dar es salaam (DSE) wawekezaji hao huziuza hisa hizo kwa bei ya juu na kupzta faida. Hii ni njia mojawapo ya kuopngeza faida kwa haraka, na hatari yha kupoteza thamani ya uwekezaji inakuiwa ndogo hasa pale wawekezaji (wanunuzi wa hisa) wanapokuwa wengi katika soko la hisa. Licha yahiyo kuna njia nyingine ambazo zinarudisha faida nzuri kwenye uwekezaji wa hisa. Mojawapo ni pale ambapo bei ya hisa kwenye soko inakuiwa imeshuka au iko chini, ila ni muhimu kufanya utafiti au kufuatilia mahesabu ya kampuni unayotaka kuwekeza au kwa kutumia wataalamu wa masuala ya fedha (financial analysts). Bei ya hisa kupanda au kushuka katika soko, ni jambo la kawaida na inasababishwa na mambo mengi. Mambo mawili makubwa ni kwamba, kampuni haifanyi vizuri na wawekezaji wake wameamua kuondoa mitaji yao kwenye hiyo kampuni na kuacha kuwekeza. Hii utaijua iwapo utakuwa unafuatilia kwa undani utendaji wa kampuni na siyo tu kuangalia bei ilioyoo sokoni. Jambo la pili ni kwamba, bei ya hisa inaendeshwa kutokana na nguvu ya soko inayoendeshwa na wanunuzi na wauzaji wa hisa. Hapa bei ya hisa inakuwa haiendani na utendaji wa kampuni. Utakuata kampuni inatengeneza faida kila mwaka na mahesabu yake yako wazi kuonyesha ufanisi wake , bado bei inakuwa chini. Huo ndio wakati mzuri wa kununua hisa kwa sababu pamoja na kwamba bei ya hisa za kampuni hiyo ziko chini ya bei iliyouzwa sokoni kwa mara ya kwanza, lakini bado kampuni inatengeneza faida. Hisa hizi zinakuwa ni nafuu na rahisi kulinganisha na thamani halisi ya hisa. Ni muhimu sana kwa wawekezaji katika hisa kusoma kwa undani mahesabu na mwenendo wa kampuni wanayotaka kuwekeza kabla ya kufanya maamuzi ya kununua au kuuza hisa zo. Kwa upande mwingine kuna hatari kwa mwekezaji kuamua kuwekeza kwenye kampuni bila ya kufanya uchunguzi yakinifu kuhusu kampuni hiyo. Kuwekeza kwenye kampuni kwa kufuata bei ya hisa tu si sahihi, mwanahisa unashauriwa kufuata uchunguzi uliofanywa na wataalamu wa kunyambulisha mahesabu ya kampuni, hii itakupa nafasi nzuri ya kujua unawekeza kwenye kampuni ya aina gani na ujtarajie mrerjesho mzuri wa mtaji uliowekeza. Kwenye kulinganisha kwamba ni kampuni gani uwekeze ni vizuri ujue mtaji wa kampuni husika, idadi ya wanahisa, idadi ya hisa zilizotolewa au zilizoko sokoni, na gharama za uendeshaji. Hapo utaweza kujua kwa nini kampuni moja inatoa gawiomla shilingi mia mbili kwa hisa na nyingine inatoa gawio la shilingi saba kwa hisa. Ni vizuri pia wanahisa kuodokana na dhana ya uwekezaji wa muda mfupi, hii itakupa msukumo hasi wa kuuza hisa kwa bei ha hasara ili kurtejesha mtaji. Uwekezaji wa muda mrefu yaani kuanzia miaka 5 na kuendelea ni uwekezaji mzuri kwani licha ya mtaji wako kuendelea kukua pia unaongeza thamani ya hisa zako kwa muda wote huo pamoja na kupata gawio la kila mwaka. Kila la heri ndugu wanahisa kwa uwekezaji bora kwenye soko la hisa. Chanzo: Mwanahisa - CRDB BANK PLC. Toleo la Novemba, 2012.

Monday, August 20, 2012

VIKWAZO DHIDI YA USINGIZI MURUA NA SULUHU ZAKE

Usingizi ni moja kati ya vitu muhmu kwa afya ya binadamu. Kukosa usingizi ipasavyo (masaa 6-8) hupelekea matatizo kama uchovu siku inayofuata, kusinzia siku inayofuata, kupungua uzito, kupungua kinga ya mwili n.k. Kuna imani potofu ya kwamba watoto ndio wanaopaswa tuu kulala muda fasaha.

Kwa kuwa watu wengi hawapo makini katika kuangalia mienendo ya maisha yao, hawawezi kujua sababu zinazopelekea matatizo hayo, hivyo kukosa sululuhu ya kudumu. Zifuatazo ni sababu zinazopekea ukosefu wa usingizi, baada ya kuzijua itakuwa rahisi kwa mtu kukabiliana na changamoto.

Kula chakula kingi muda mchache kabla ya kulala.

Kula chakula kingi, hususani nafaka, muda mfupi kabla ya kulala hufanya mwili utumie nishati nyingi katika kumeng'enya chakula, hivyo kuvuruga utaratibu wa nishati wa mwili. Pia kunywa maji kabla ya kulala humfanya kuamka usiku ili kujisaidia, hivyo kubadili utaratibu wa usingizi.
Mtu anapaswa kula chakula chepesi na maji kidogo angalau nusu saa kabla ya kulala.

Kulala mazingira duni.

Kulala katika mazingira yanayokinzana na utu wa mtu huvuruga utaratibu wa mwili. Mazingira kama; chumba chenye mwanga mkali, chumba chenye joto au baridi kali, kulala kwenye kelele, kulala kwenye godoro laini au gumu sana, chumba kisicho na hewa safi ya kutosha n.k humfanya mtu kukosa usingizi.

Kubadili mfumo wa maisha.

Kubadili mfumo wa maisha na ambao ulikuwa umezoelewa na mwili hutatiza usingizi. Kwa mfano; kumpoteza ndugu au rafiki wa karibu, kuanza kazi mpya, kufanya kazi ngumu, kuingia kwenye ndoa, kuwa na msongo mawazo n.k huwafanya watu wengi kukosa usingizi.
Hali hii huchukua siku chache, ikiwa kama ukosefu wa usingizi itachukua muda mrefu, mtu anapaswa kufanya tahtmini ya kina.

Mazingira duni ya kijamii.

Mazingira duni ya kijamii kama; kulala zaidi ya mtu mmoja kwenye kitanda kimoja, kulala na mtu msumbufu hususani mtoto mdogo, kulala chumba kimoja na mtu anayekoroma, kulala na mtu anayesumbua usiku, kulala chumba chenye wadudu kama chawa, kunguni, viroboto n.k.
Mazingira haya yanasababishwa na umasikini wa kipato.

Matumizi ya madawa.

Kuna aina nyingi sana ya madawa ya hosptalini ambayo, pamoja na kutibu au kupunguza maumivu, hupelekea kukosekana kwa usingizi. Madawa hayo ni kama madawa ya kupunguza maumivu, kupunguza mawazo, madawa ya usingizi n.k.
Mtu anapaswa kusoma maelekezo au kupata ushauri wa daktari kabla ya kutumia dawa yoyote ile ili apate kujua madhara yake na jinsi ya kuyakabili.

Matumizi ya vinywaji baridi na sigara muda mchache kabla ya kulala.

Vinywaji baridi vina kokaini, chai au kahawa ambayo huongeza msukumo wa damu. Matumizi ya vinywaji hivyo kabla ya kulala kukatiza usingizi. Kwa upande wa sigara, ikilinganishwa na watu wasiovuta sigara, watu wanaovuta sigara hukawia kupata usingizi, hivyo, kupata masaa machache ya kulala.
Kuna watu wamezoea kunywa pombe ndipo wapate usingizi, watu hawa ni watumwa wa pombe na wengi wao hutumia pombe kali, baada ya muda, pombe haitoweza kumsabishia usingizi kabiasa au akiwa hana hela ya kununua pombe mtu huyo hatoweza kulala.

Kwa kiasi kikubwa, sababu za ukosefu wa usingizi zipo chini ya uwezo wa binadamu, hivyo, mtu mmoja mmoja na jamii kwa ujumla inapaswa kutengeneza mazingira yanayopekekea usingizi murua, mafanikio ya mtu katika kazi za kujiletea maendeleo, hutegemea, pamoja na mambo mengine, kiasi cha mapumziko anayopata kila siku kupitia usingizi.

Monday, August 13, 2012

MUUNDO WA MPANGO WA MAENDELEO

Watu wengi hushindwa kufikia malengo waliyojiwekea kwa kuwa, moja ya sabau ni, kushindwa kupanga. Kushindwa kupanga hupelekea kushindwa kutekeleza hivyo malengo kutikiwa. Zifuatazo ni hatua muhimu za kumsadia mtu pindi apangapo mradi wa maendeleo.

1. Kununua kitabu cha mipango. Mtu anapaswa kununua kitabu kidogo kwa ajili ya kuratibu na kutunza kumbukumbu za kila siku za mtu binafsi. Vitabu hizi vipo takribani kila duka la vifaa vya shule na ofisini, hujulikana kama "diary" kwa lugha ya Kiingereza.

2. Kuandika mtizamo, lengo au matarajio ya mradi husika. Mtu anapaswa kuandika mradi wake kwenye ukurasa wa kwanza wa kitabu cha mipango. Lengo husika linapaswa kuandikwa kwa herufi kubwa na kwa lugha fasaha. Kwa mfano, LAZIMA NIANZISHE MRADI WA UFUGAJI WA KUKU WA KIENYEJI IFIKAPO MWEZI JANUARI MWAKANI . Mtu anapaswa kuhakikisha anaandika lengo moja tu! Ili iwe rahisi kutekeleza.

3. Kuandika kwa kifupi shughuli muhimu zitakazofanyika na muda mahususi wa kuzifanya ili kufikia lengo kuu. Shughuli hizo hujumuisha malengo madogo madogo. Kwa mfano:

Ni lazima nianzishe mradi wa ufugaji wa kuku wa kienyeji kabla ya mwezi Januari mwakani. Ili kufanya hivyo ninapaswa kufanya yafuatayo; (i) kuomba ushauri kutoka kwa mfugaji maarufu wa kuku wa kienyeji juu ya gharama muhimu wiki ya tatu ya mwezi Agosti (ii) kukamilisha gharama muhimu za kuanza mradi kabla ya wiki ya nne ya mwezi Agosti, kama ikibidi (iii) kuomba ushauri kutoka kwa Afisa Mifugo juu ya aina bora ya kuku, magonjwa n.k wiki ya kwanza ya mwezi Septemba (iv) kufanya utafiti juu ya upatikanaji wa soko la kkienyeji ndani ya wiki ya pili na tatu ya mwezi Septemba (v) kuanza kujenga banda wiki ya tatu ya mwezi Septemba na kukamilisha kabla ya mwisho wa mwezi Oktoba (vi) kununua chakula na dawa muhimu wiki ya kwanza na ya pili ya mwezi Novemba (vii) kununua kuku wa kienyeji; mitetea nane na jogoo mmoja wiki ya kwanza ya mwezi Desemba. Hivyo kuanza ufugaji rasmi kabla ya mwezi Januari.

Mpangilo wa shughuli na muda hutegemea mazigira, uelewa wa mtu, rasilimali akizo nazo n.k. Kwa mfano, kupata mtaji kwa mtu mmoja ikawa changamoto ili hali, kwa mtu mwinine kupata ushauri ikawa changamoto kuu.Mtu apange shughuli rahisi kisha shughuli ngumu baadaye kadiri ya uwezo wake. Ni bora kumshirikisha mtu wa karibu ambaye nimzoefu wakati wa kupanga ili kuepuka kupanga shughuli isiyotekelezeka ndani ya muda fulani.

4. Kurudia kusoma, kufanya marekebosho na kukariri mwongozo ulioandaliwa. Muongozo uwekwe maeneo ambayo ni rahisi kuuona na kuusoma kama kwenye pochi au kwenye mkoba. Hii itaongeza hamasa ya kusoma na kutaka utekelezaji.

5. Kuanza utkelezaji kwa kuandaa ratiba ya hughuli iliyopangwa kufanyika ndani ya muda husika. Katika hatua hii mtu anapaswa kuwa makini sana ili asiruke shughuli aliyoipanga. Ikiwa kama shughuli husika haikuisha ndani ya muda uliopangwa, basi ipelekwe mbele. Kuruka hatua kutasababisha kuvuruga mpango mzima.

6. Kufanya uchambuzi wa hatua kwa hatua. Mtu anapaswa kuangalia utekelezwaji hatua iliyopita ili kufanya marekebisho kwa hatua zitakazofuata kabla mambo hayajawa magumu. Mwenye mradi anapaswa kuwaongoza kwa makini wasaidizi wake wa kila siku.

Monday, August 6, 2012

VIASHIRIA VYA BAHATI

Watu wengi hufikiri ya kwamba bahati (nzuri au mbaya) hujijia tu, haibashiriki na ni vigumu kuzuia. Hiyo ni kwa kuwa hawajui maana halisi ya bahati. Ikiwa kama mtu hajui maana halisi ya bahati ni vigumu kuitawala. Waswahili wanasema "mtembea bure si sawa na mkaa bure" pia "bahati ya mbwa ipo kwenye miguu yake".

Bahati ni kujitambua dhidi ya uhalisia. Bahati ni kuwa na hisia chanya juu ya tukio au jambo fulani. Mtu mwenye hisia chanya huona kila kitu kinamtumikia (kila kitu kinamsadia kufanikiwa), kwa upande mwingine, mtu mwenye hisia hasi huona kila kitu kinampiga vita; kila kitu huonekana ni kikwazo.

Kiasi cha imani (nguvu itokayo ndani) huamua kiwango cha hisia na bahati ya mtu. Mtu anapofanya jambo lolote pasipo imani, kufanya jambo kwa mashaka makubwa, huwa na uwezekano mkubwa kufanya makosa ya kizembe hivyo kujiweka katika nafasi kubwa ya kungeza vikwazo au kukosa kabisa kile alichotaka. Pindi mtu anapojiamini kwa kiasi kikubwa ndipo uwezekano wa bahati (kufanikiwa) unapoongezeka.

Kwa kiasi fulani, bahati hutegemea maarifa. Mtu mwenye maarifa hufanya kazi kwa uhuru. Ni vigumu kutenganisha bahati na maarifa; kwani ili kufanya kitu kwa usahihi uwezo wa mtu husika kufuata sheria na kanuni ipasavyo unahitajika.

Kwa kuwa bahati hutegemea imani, mtu anapaswa kuwa makini na kiwango cha imani yake wakati anapofanya jambo lolote lile. Ikiwa kama kiwango cha imani ni kidogo, yafaa kusitisha kufanya jambo hilo, au kufanya hatua kwa hatua na kwa umakini mkubwa kama haiwezekani kusitisha shughuli husika.

Watu wanaolazimisha kufanya jambo bila ya imani nalo hujikuta wakifanya makosa bila ya kujitambua, kusahau hatua za kufuata, kushindwa kujitetea pindi wanapotakiwa kijitetea, hivyo kubaki wakijilaumu kwa kujisemea "nina bahati mbaya".

Kukosa umakini kimawazo huwafanya watu kudharau mambo ya msingi; kujikuta wakifanya mambo wasiyotayatarajia kisha kutokufanikiwa. Ili kuongeza nafasi ya bahati ya kufanikiwa yapaswa kuwekeza kimawazo, kushirikisha maarifa kwenye kazi ifanyikayo kwa wakati husika. Kuwekeza kimawazo husaidia kutumia rasilimali kwa ufanisi zaidi.

Takribani watu wote (wanasayansi mashuhuri, wafanyabiashara wakubwa, wasomi n.k) waliofanikiwa, walifanikiwa kwa kuwa kiwango chao cha imani kilikuwa juu. Kufanya kazi bila ya i tiketi ya kushindwa. Mtu anayetaka bahati nzuri huchagua mtizamo chanya, mtizamo chanya huongeza nishati na kusadia jitihada za kufanikiwa.

Kila mtu anayo nafasi ya kufanikiwa, watu wengi hawajui maana na jinsi ya kulinda nafasi wanazopata katika maisha. Bahati nzuri ipo, na kila mtu anao uwezo wa kuitawala. Kwa kulitambua hilo, hakuna haja ya kuogopa kufanya jambo lolote kwa kuwa hakuna bahati mbaya.

Monday, July 30, 2012

MIKAKATI YA KUONDOKANA NA MAPENZI YA JINSIA MOJA

Idadi ya watu wanaojihusisha na mapenzi ya jinsia moja inaongezeka kwa kasi. Nchi kadhaa, hususani za Ulaya na Marekani zimehalalisha 'ndoa' za aina hiyo kwa kigezo cha haki za binadamu, huku zikizishinikiza nchi changa kufanya hivyo.
Wanaume wanaojihusisha na mahusiano ya kimapenzi na wanaume wenzao wanaitwa mashoga, huku wanawake wakiitwawasagaji. Kuna baadhi ya mashoga na wasagaji wasiopenda hali yao ya kimapenzi ila hawajui wataachaje. Zifuatazo ni baadhi ya mbinu za kuondokana na uovu huu.

1. Kutafakari mpango wa Mungu.

Kila shoga au msagaji anapaswa kutafakari azma ya Muumba wake; azma ya Mungu itafakariwe sambamba na matendo anayotenda. Mungu alimuumba mtu mme na mtu mmke ili wazaliane, kumheshimu na kumtukuza. Mungu hakumuumba mtu ili amwoe mtu wa jinsia yake, na kufanya hivyo ni kukiuka maagizo ya Mungu, na hakuna msamaha kwa mtu anayevunja amri ya Mungu. Kwenda kinyume na mpango wa Mungu ni usaliti, adhabu ya usaliti ni kubwa sana.

2. Kuomba msaada kutoka kwa wataalamu.

Kuondokana na hali ya ushoga au usagaji kunawezekana ikiwa kama kila mshiriki ataomba ushauri na tiba, hususani tiba ya akili, kutoka kwa wataalamu wa saikolojia. Pia viongozi wa dini wanao mchango mkubwa sana, kwani, kwani wanauwezo wa kutoa mafunzo ya hatua kwa hatua, kulingana na imani ya mwathirika hata atapopona. Mtu husika anapaswa kuvunja ukimya.

3. Kuweka dhamira ya kuacha.

Hakuna lisilowezekana chini ya jua. Ikiwa kama mshiriki wa mahusiano ya jinsia moja atadhamiria kwa dhati kuacha, atafanikiwa. Kufanikiwa au kutafanikiwa kunategemeana na maamuzi ya mtu. Shoga au msagaji anapaswa kufanya magumu kwa kutumia msaada kutoka kwa watu wa karibu; watu wanaotoa msaada wa hali na mali na kwa mapenzi mema.

4. Kukwepa mazingira hatarishi.

Shoga au msagaji anapaswa kukwepa mazingirompa vishawishi, ikiwamo kuwakwepa mashoga au wasagaji, kukwepa m,aeneo aliyokuwa akikutana na wenzake, na kupenda kukaaa maeno yanayotumiwa watu wa jinsia zote. Marafiki na mazingira huwafanya watu kuingia maovuni, vivyo hivyo, huwafanya watu kukwepa uovu.

5. Kujiamini

Shoga au msagaji napaswa kujenga utashi kutoka ndani. Utashi imara unategemea mawazo chanya juu ya jambo husika. Manneno yanohusiana na udhaifu na kukata tamaa hayatakiwi kabisa; maneno kama "siwezi kuacha...", hatatakiwi kabisa. Maneno ya ujasiri na kujikupewa kipaumbele muda wote, maneno kama "mimi ni mwanamke, mimi ni fahari ya ulimwengu nitadhihirisha hivyo kwa kuacha usagaji", "wanaume hawashindwi na kitu, mimi ni mwanaume, mini sitoshindwa kuacha ushoga".

6. Kuangalia vivutio vya jinsia tofauti

Msagaji anapaswa vivutio bna thopata mwananmke asiye msagaji kutoka kwa jamii, pia vivutio kutoka kwa mwanaume kama sauti, misuli n.k pia shoga anapaswa kungaliasio mashoga, vivutio kutoka kwa mwanamke kama sura, mwendo n.k. Jinsia zote mbili zri thamani ya kulea familia katika maadili mema, kuwa na watoto na kuitwa baba au mama.

7. Kutolaumu matukio ya siku za nyuma.

Matukio kama unyanyasaji wa kijinsia aliowahi kufanyiwa mtu siku za nyuma, hususani wakati wa utoto, huleta changamoto katika kuacha kile mtu anachoamini mtu kinampa furaha. Ikiwa kama shoga aliwahi kunyanyaswa kijinsia, anapaswa kuamini ya kwamba aliyefanya hivyo alitumwa na shetani, na ni sehemu ya mapito ya mwanadamu.

8. Kusoma kutoka kwa walioshinda

Kuna simulizi na machapisho mengi kutoka kwau waliofanikiwa kuepa uovu huu. Mshiriki anapaswa kusoma ili kuipata mbinu bora zaidi, ikiwa ni pamoja na kuombna ushauri pale anapokumbana na changamoto kubwa; changamoto inayotishia kuzima juhudi zake za kuacha. Kupitia Google kuna toviuti za mashirika au vikundi vingi vinavyojihusisha na kuwasaidia watu wanaoshiriki mapenzi ya jinsia moja ili waweze kuacha.
KILA KITU KINAWEZEKANA, KUACHA MAPENZI YA JINSIA MOJA INAWEZEKANA!

Monday, July 23, 2012

MISINGI YA KUWALINDA WATOTO DHIDI YA MAPENZI YA JINSIA MOJA

Janga la mahusiano ya kimapenzi baina ya watu wa jinsia moja ni changamoto kubwa sana katika malezi ya watoto. Kwa kiasi kikubwa mapenzi ya jinsia moja huchangiwa na sababu za kimazingira na chaguo la mtu husika. Japokuwa, kwa kiasi kidogo, aina hii potofu ya mahusiano inachangiwa na sababu za kibailojia.
Hali ilikuwapo kabla hata ya kuzaliwa Yesu Kristo. Yote kwa ypote, ni lazima kupambana na hali hii na kuishinda. Misingi ifuatayo yafaa kutumiwa na wazazi, walezi na jamii kwa ujumla ili kuwalinda watoto dhidi ya janga la mahusiano ya kimapenzi ya jinsia moja.

1. Kuwalinda watoto dhidi ya unyanyasaji wa kijinsia.

Wazazi na walezi wanapaswa, kwa nguvu zao zote, kuhakikisha usalama wa watoto. Kuwalinda watoto wasitendewe unyama dhidi ya jinsia yao kama kama ulawiti na ubakaji.

Kwa mfano, mtoto wa kike aliyebakwa hujenga chuki dhidi ya wanaume, hivyo hukua na hasira dhidi ya mwanaume yeyote yule hata atakapokuwa mkubwa. Kutokana na chuki dhidi ya wanaume, mtoto huyo huimarisha mahusiano hususani ya kimapenzi dhidi ya wasichana mwingine mwenye chuki dhidi ya wanaume kama alivyo yeye. Lengo la kufanya hivyo ni kutaka kutimiza mahitaji yao ya kimapenzi.

Unyanyasaji mkubwa wa kijinsia hufanyika majumbani; unyanyasaji wa kijinsia hufanywa na watu wanaoheshimika kama baba wa kambo, baba mdogo, mjomba, shangazi, mfadhili n.k. Hivyo, wazazi na walezi wanapaswa kuwa makini sana dhidi ya watu wanaoishi au kuwalea watoto wao.

2. Kuwakuza watoto katika jinsia zote.

Wazazi ndio shule ya kwanza kwa watoto. Watoto hujifunza kutoka kwa wazazi maana na majukumu ya baba na mama (au mme na mke).
Hivyo, baba anapaswa kuwa mfano mzuri wa kuigwa kwa watoto wa kiume, na mama kuwa mfano mzuri wa kigwa kwa mtoto wa kike kupitia maisha yao ya kila siku.

Ikiwa kama ni vigumu kwa mzazi mmoja kushiriki katika malezi, mtoto wa jinsia husika atengewa mazingira yatakayomwezesha kuiga na kuishi kadiri ya jinsia yake. Kwa mfano, kupata nafasi ya kuona jinsi familia za jirani zinavyoishi.

3. Kutomkaripia mtoto vikali kutokana na tabia yake.

Wazazi na walezi wananapaswa kuwa makini pale wanapowaonya watoto wao kwa kuwa wameonyesha tabia au mienendo hatarishi. Kwa mfano, kutompiga vikali mvulana kwa kuwa anajiremba au kuiga sauti za wasichana.
Makaripio makali huwafanya watoto kukubuhu na kujenga kiburi, na hivyo kuamua kuendeleza tabia husika.

Wazazi na walezi wanapaswa kujua ya kwamba watoto, hususani wakati wa balehe au kuvumja ungo, ni watundu sana na hupenda kuiga kila kitu. Hivyo, wazazi na walezi wanapaswa kuwa na upole huku wakiwafundisha madhara ya tabia hatarishi.

4. Kutoa fursa sawa kwa jinsia zote za watoto.

Watoto huwa njiapanda nyingi hususani wakati wa balehe au kuvunja ungo. Baadhi ya watoto huona ya kwamba jinsia tofauti na yao inapata faida sana. Hivyo huanza kuiga mitindo yao ya maisha, mingi ya mitindo hiyo ikiwa ni hatarishi.

Kwa mfano, watoto wa kike huona watoto wa wakipewa uhuru wa kwenda watakapo, kutopangiwa majukumu au kazi nyingi za kifamilia n.k. Hivyo, wasichana hao huiga mienendo ya kiume ili kujiridhisha. Tabia hii ikiachwa huwafanya wasichana hao kujihususisha kimapenzi na wasichana wenzao. Wazazi na walezi wanapaswa kutoa fursa sawa kwa wote ili watoto wote wafurahie jinsia zao tangu awali.

5. Kuwalea watoto kwa misingi ya dini.

Wazazi na walezi wanapaswa kuwalea watoto kwa misingi ya imani zao. Ili kufanikisha hilo, wazazi na walezi wanapaswa kuishi kandiri ya imani zao ya kila siku.
Malezi ya kidini huwafanya watoto kuona muhimu wao kwa mujibu wa jinsia zao.

Kwa mfano, wazazi kuwasimulia watoto habari za watu maarufu waliomtumikia Mungu katika dini husika kwa jinsia. Pia kuwaambia watoto ya kwamba Mungu alimuumba mtu mke na mtu mme ili wamtumikie.

6. Kuwalea watoto kwa mujibu wa jinsia zao.

Mtoto wa kiume anapaswa kulelewa kama mtoto wa kiume ili aweze kuwa mwanaume, na mtoto wa kike vivyo hivyo. Hata kama mtowazazi waliyoipendelea, mtoto aliyezali maadili mema na mwenendo unaokubalika.

Kwa mfano, ikiwa wazazi walipendelea mtoto wa kwanza awe wa kike, na akazaliwa mtoto wa kiume; wanapaswa kumlelea mtoto huyo kama wa kiume, na si kumdekeza. Watoto wengi wa kiume wanaodekezwa huwa mashoga.

Ikiwa kama wazazi na walezi (jamii kwa ujumla) watafanikiwa kuwalea watoto kwa misingi hiyo; kabla ya mtoto kuanza maisha tofauti na ya familia, kwa mfano kwenda shule ya kulala (bodi), changamoto ya mapenzi ya jinsia moja itakuwa imepunguzwa au kumalizika kabisa. Takwimu zinaonyesha kwamba watu wenye mahusiano ya jinsia huimarika wakiwa chini ya umri wa miaka 18.

Monday, July 16, 2012

MBINU ZA KUUKABILI USHIRIKINA

Ushirikina ni hali ya kuamini kuna haja ya kuwa na nguvu ya ziada kutoka kwa mtu au nafsi ili kuweza kufanikisha jambo fulani. Kwa mfano, kuamini kuna haja ya kufanya kafara (kuchinja na kumwaga damu ya mtu au mfugo) ili kuweza kupata kazi. Imani za ushirikina ni maarufu katika jamii na sehemu mbalimbali duniani.

Imani za ushirikina ni kukwazo kikubwa kwa jamii nyingi kwa kuwa:

Hupunguza nafasi za kusoma. Kuamini katika ushirikina kutochukua jitihada za kusoma ili kupata suluhu juu ya changamoto zinazoikabili jamii husika. Kwa mfano, kutegemea ushirikara kunaweza kuwazuia wafanyabiashara kutofanya tafiti mpya juu ya mwenendo wa biashara, hatimaye hufilisika.

Huongeza mzigo. Kuamini ushirikina kunamfanya mtu kuishi akiwa amevaa vitu mbalimbali ili kutimiza malengo, mfano, kuvaa irizi. Vitu hivyo kwa ujumla wake huongeza mzigo katika mwili wa mtu.

Huzuia malengo kutimia. Watu wanaoamini ushirikina huacha kufanya mambo waliyoyapanga kwa kuwa masharti hayaruhusu. Kwa mfano, mtu anayekwenda kufanya biashara fulani, akikutana na bundi asubuhi, kwa kuwa anaamini bundi ni ishara ya mkosi, mtu huyo hurudi nyumbani, hivyo, kuacha kufanya biashara kwa siku husika.

Huleta mfadhaiko. Ikiwa kama mtu anaamini irizi ndio kinga yake, kwa bahati mbaya akasahau kuvaa irizi siku fulani, siku hiyo ataishi kwa wasiwasi na hofu siku nzima. Au mtu akiamini mzee fulani ni mchawi, na akakutana nae, mtu huyo hupata mfadhaiko kwa kuogopa atakuwa amelogwa.

Huongeza changamoto za kimaisha. Kutokana na kuamini ushirikina, mshirikina hujinyima fursa nyingi za kusonga mbele. Kwa mfano, mtu anayeamini ya kwamba jirani yake ni mchawi, mtu huyo hukatisha mawasiliano na jiarani yake, pia, mtu huyo anaweza kuwaacha watoto wake bila ya uangalizi wowote kwa kuogopa wanawe watalogwa na jirani yake.

Mbinu za Kukabili Imani na Madhara ya Ishirikina.

Inawezekana kabisa kuepa ushirikina, na mtu husika asidhurike kwa kufanya yafuatayo:
Kutumia takwimu.
Ili kukwepa mawazo au uhusishwaji wa tukio fulani na imani za kishirikina, mtu anapaswa kusoma takwimu dalili n.kuhusu tukio husika. Kwa mfano, ili kutohusisha kifo na ushirikina, mtu anapaswakusoma takwimu kuhusiana na kifo cha mtu husika.

Kutafuta ushauri.
Ili kupunguza uwezekano wa madhara fulani kutokea mtu anapaswa kuomba na kufuata ushauri kutoka kwa wataalamu. Kwa mfano, ili kukwepa hasara katika biashara, mfanyabiashara anapaswa kutafuta na kutekeleza ushauri kutoka kwa wataalamu wa biashara kabla na wakati wa biashara husika.

Kujaribu nguvu ya ushirikina.
Ikiwa kama mtu anaamini ya kwamba bila ya kuwa na irizi hawezi kufanya vizuri katika mchezo, mtu huyo afanye maandalizi sahihi huku akiwa na imani ya kuwa atafanikiwa bila ya kukumia kizizi. Pia mtu huyo anaangalie kama mara zote anazotumia irizi je anakiwa? Kama kizizi ndio suluhu ya kufanikiwa, je kuna haja gani ya kufanya mazoezi?

Kumwamini Mwenyezi Mungu.
Kila kitu (kinachoonekana au kisichoonekana) kimeumbwa na Mungu. Mungu ndiye mtawala wa kila kitu. Ikiwa kama Mwenyezi Mungu ameweza kuumba kila kitu, je atashindwaje kushinda hila za ushirikina?

Ikiwa kama mambo hayaendi kama mtu alivyopanga, haimaanishi ya kwamba Mungu ameshindwa, bali kwa namna moja au nyingine Mungu anatoa somo. Kwani kutokana na matatizo yanayomkabili mtu, ndipo watu huamini na kutii uwepo wa Mungu. Kupiga magoti kwa Mungu na kufanya kazi kwa bidii ndiko kunakoleta suluhu ya kudumu.

Achilia mbali mila na tamaduni, imani za ushirikina zinachukua nafasi kubwa katika jamii kwa kuwa watu hawana suluhu dhidi ya changamoto zinazowakabili. Kwa mfano, kukosekana kwa elimu na tiba juu ya ugonjwa fulani unaosababisha vifo vingi, huwafanya watu katika jamii husika kuhusisha ugonjwa huo moja kwa na imani za ushirikina.