Monday, January 2, 2012

MBINU ZA KUFANIKIWA WAKATI WA USHAWISHI

Kushindwa kushawishi kumewafanya watu wayaone maisha ni adhabu. Kushindwa kushawishi kumewaangusha wengi katika ulimwengu huu; ulimwengu unaokwenda kwa kasi ya ajabu.

Si rahisi kumshawishi mtu akubali ombi na kutoa huduma au msaada kwa mtu mwingine. Kazi hii ngumu inaweza kufanikishwa kwa kutumia mbinu tano rahisi. Mbinu hizo ni zifuatazo:

Mbinu I. Kwenda sambamba na mshawishiwa.
Mshawishi anapaswa kutazama kwa makini jinsi mshawishiwa anavyowasiliana; iliwa ni pamoja na matumizi ya lugha ya ishara, ili naye afanye vivyo hivyo.

Ingawaje, mshawishi anapaswa kuwa makini ili asionekane anamkebehi mshawishiwa. Ikiwa mshawishiwa atagundua kuna "usanii" hatotia maanani yale anayoambiwa na hatimaye kutokubali kutimiza ombi la mshawishi.

Mbinu II. Kutimiza mahitaji ya wakati husika.
Watu hujipendelea. Watu hupenda mahitaji yao yatimizwe kwanza ndipo ya wengine yafuate. Mshawishi atambue vipaumbele vya msahwishiwa atakavyotekeleza ili maombi yake yatimizwe kwa urahisi.

Mshawishi atizame mahitaji, matakwa, vionjo n.k ili aweze kuvuta hisia za mshawishiwa. Mshawishi ajitahidi kutimiza kero au matakwa ya mshawishiwa kwa kadiri ya maadili, hali na uwezo wake kabla ya kutoa ombi lake.

Mbinu III. Kutoa uthibitisho.
Mshawshi atoe uthibitisho unaoonyesha ya kwamba ombi au lengo lake litatelelezeka bila ya vikwazo vingi. Mshawishi atoe uthibitisho pasipo na shaka ya kwamba atatoa "bidhaa" bora baada ya muda husika; baada ya ombi lake kukubaliwa na kutekelezeka.

Mshindani ashindanishe uthibitisho wake dhidi ya washindani wengine. Mshawishi ahakikishe anayosema au kutoa ni ya kweli na yanawezekana. Msahwishi aonyeshe uhusika au nafasi yake huku akitabasamu ili kukuza imani na urafiki. Pia mshawishi aonyeshe ya kwamba yupo tayari kutoa msaada wa ziada kama ikibidi kufanya hivyo.

Mbinu IV. Kuwasiliana kwa ufasaha.
Takribani watu wote wanapenda wakubalike na na kueleweka kadiri wanavyohisi ni sahihi, kwa kadiri ya hisia zao bila kujali jinsi wanavyowasiliana. Mshawishi anapaswa kujiuliza, je niwasilisheje ombi langu bila ya kumkwaza mshawishiwa?

Ili kufanya hivyo, mshawishi anapaswa kutumia mbinu za mawasiliano bora zilizoandika katika mada mbili zilizopita. Mshawishi atambue na kukwepa maneno ambayo huathiri hasi utu wa mtu au jamii husika kama yasipotumika kwa kuzingatia mazingiza na aina ya mazungumzo.

Mbinu V. Kukubaliana na mshawisiwa.
Takribani watu wote hupenda au huridhika kwa kuambiwa "nimekuelewa". Katika hili mshawishi ahakikishe anasikiliza kwa makini na kukubali mawazo yanayofanikisha ombi lake likubalike.
Mshawishi akubaliane pia mawazo kinzani kabla ya kukosoa au kutoa ufafanuzi. Kwa mfano, "unaweza kuwa sahihi lakini ni bora kama ingekuwa hivi......", "natambua hali halisi lakini nitafanya hivi....ili kuweka mambo sawa"

Mshawishi ahakikishe ya kwamba pindi ombi lake litapokubaliwa na kutekelezeka pande zote mbili zitafanikiwa; ili mshawishiwa akubali kutoa msaada. Mshawishiwa atatoa msaada na ushirikiano pale atakapohisi anafanya uamuzi sahihi.

No comments:

Post a Comment