Monday, July 30, 2012

MIKAKATI YA KUONDOKANA NA MAPENZI YA JINSIA MOJA

Idadi ya watu wanaojihusisha na mapenzi ya jinsia moja inaongezeka kwa kasi. Nchi kadhaa, hususani za Ulaya na Marekani zimehalalisha 'ndoa' za aina hiyo kwa kigezo cha haki za binadamu, huku zikizishinikiza nchi changa kufanya hivyo.
Wanaume wanaojihusisha na mahusiano ya kimapenzi na wanaume wenzao wanaitwa mashoga, huku wanawake wakiitwawasagaji. Kuna baadhi ya mashoga na wasagaji wasiopenda hali yao ya kimapenzi ila hawajui wataachaje. Zifuatazo ni baadhi ya mbinu za kuondokana na uovu huu.

1. Kutafakari mpango wa Mungu.

Kila shoga au msagaji anapaswa kutafakari azma ya Muumba wake; azma ya Mungu itafakariwe sambamba na matendo anayotenda. Mungu alimuumba mtu mme na mtu mmke ili wazaliane, kumheshimu na kumtukuza. Mungu hakumuumba mtu ili amwoe mtu wa jinsia yake, na kufanya hivyo ni kukiuka maagizo ya Mungu, na hakuna msamaha kwa mtu anayevunja amri ya Mungu. Kwenda kinyume na mpango wa Mungu ni usaliti, adhabu ya usaliti ni kubwa sana.

2. Kuomba msaada kutoka kwa wataalamu.

Kuondokana na hali ya ushoga au usagaji kunawezekana ikiwa kama kila mshiriki ataomba ushauri na tiba, hususani tiba ya akili, kutoka kwa wataalamu wa saikolojia. Pia viongozi wa dini wanao mchango mkubwa sana, kwani, kwani wanauwezo wa kutoa mafunzo ya hatua kwa hatua, kulingana na imani ya mwathirika hata atapopona. Mtu husika anapaswa kuvunja ukimya.

3. Kuweka dhamira ya kuacha.

Hakuna lisilowezekana chini ya jua. Ikiwa kama mshiriki wa mahusiano ya jinsia moja atadhamiria kwa dhati kuacha, atafanikiwa. Kufanikiwa au kutafanikiwa kunategemeana na maamuzi ya mtu. Shoga au msagaji anapaswa kufanya magumu kwa kutumia msaada kutoka kwa watu wa karibu; watu wanaotoa msaada wa hali na mali na kwa mapenzi mema.

4. Kukwepa mazingira hatarishi.

Shoga au msagaji anapaswa kukwepa mazingirompa vishawishi, ikiwamo kuwakwepa mashoga au wasagaji, kukwepa m,aeneo aliyokuwa akikutana na wenzake, na kupenda kukaaa maeno yanayotumiwa watu wa jinsia zote. Marafiki na mazingira huwafanya watu kuingia maovuni, vivyo hivyo, huwafanya watu kukwepa uovu.

5. Kujiamini

Shoga au msagaji napaswa kujenga utashi kutoka ndani. Utashi imara unategemea mawazo chanya juu ya jambo husika. Manneno yanohusiana na udhaifu na kukata tamaa hayatakiwi kabisa; maneno kama "siwezi kuacha...", hatatakiwi kabisa. Maneno ya ujasiri na kujikupewa kipaumbele muda wote, maneno kama "mimi ni mwanamke, mimi ni fahari ya ulimwengu nitadhihirisha hivyo kwa kuacha usagaji", "wanaume hawashindwi na kitu, mimi ni mwanaume, mini sitoshindwa kuacha ushoga".

6. Kuangalia vivutio vya jinsia tofauti

Msagaji anapaswa vivutio bna thopata mwananmke asiye msagaji kutoka kwa jamii, pia vivutio kutoka kwa mwanaume kama sauti, misuli n.k pia shoga anapaswa kungaliasio mashoga, vivutio kutoka kwa mwanamke kama sura, mwendo n.k. Jinsia zote mbili zri thamani ya kulea familia katika maadili mema, kuwa na watoto na kuitwa baba au mama.

7. Kutolaumu matukio ya siku za nyuma.

Matukio kama unyanyasaji wa kijinsia aliowahi kufanyiwa mtu siku za nyuma, hususani wakati wa utoto, huleta changamoto katika kuacha kile mtu anachoamini mtu kinampa furaha. Ikiwa kama shoga aliwahi kunyanyaswa kijinsia, anapaswa kuamini ya kwamba aliyefanya hivyo alitumwa na shetani, na ni sehemu ya mapito ya mwanadamu.

8. Kusoma kutoka kwa walioshinda

Kuna simulizi na machapisho mengi kutoka kwau waliofanikiwa kuepa uovu huu. Mshiriki anapaswa kusoma ili kuipata mbinu bora zaidi, ikiwa ni pamoja na kuombna ushauri pale anapokumbana na changamoto kubwa; changamoto inayotishia kuzima juhudi zake za kuacha. Kupitia Google kuna toviuti za mashirika au vikundi vingi vinavyojihusisha na kuwasaidia watu wanaoshiriki mapenzi ya jinsia moja ili waweze kuacha.
KILA KITU KINAWEZEKANA, KUACHA MAPENZI YA JINSIA MOJA INAWEZEKANA!

Monday, July 23, 2012

MISINGI YA KUWALINDA WATOTO DHIDI YA MAPENZI YA JINSIA MOJA

Janga la mahusiano ya kimapenzi baina ya watu wa jinsia moja ni changamoto kubwa sana katika malezi ya watoto. Kwa kiasi kikubwa mapenzi ya jinsia moja huchangiwa na sababu za kimazingira na chaguo la mtu husika. Japokuwa, kwa kiasi kidogo, aina hii potofu ya mahusiano inachangiwa na sababu za kibailojia.
Hali ilikuwapo kabla hata ya kuzaliwa Yesu Kristo. Yote kwa ypote, ni lazima kupambana na hali hii na kuishinda. Misingi ifuatayo yafaa kutumiwa na wazazi, walezi na jamii kwa ujumla ili kuwalinda watoto dhidi ya janga la mahusiano ya kimapenzi ya jinsia moja.

1. Kuwalinda watoto dhidi ya unyanyasaji wa kijinsia.

Wazazi na walezi wanapaswa, kwa nguvu zao zote, kuhakikisha usalama wa watoto. Kuwalinda watoto wasitendewe unyama dhidi ya jinsia yao kama kama ulawiti na ubakaji.

Kwa mfano, mtoto wa kike aliyebakwa hujenga chuki dhidi ya wanaume, hivyo hukua na hasira dhidi ya mwanaume yeyote yule hata atakapokuwa mkubwa. Kutokana na chuki dhidi ya wanaume, mtoto huyo huimarisha mahusiano hususani ya kimapenzi dhidi ya wasichana mwingine mwenye chuki dhidi ya wanaume kama alivyo yeye. Lengo la kufanya hivyo ni kutaka kutimiza mahitaji yao ya kimapenzi.

Unyanyasaji mkubwa wa kijinsia hufanyika majumbani; unyanyasaji wa kijinsia hufanywa na watu wanaoheshimika kama baba wa kambo, baba mdogo, mjomba, shangazi, mfadhili n.k. Hivyo, wazazi na walezi wanapaswa kuwa makini sana dhidi ya watu wanaoishi au kuwalea watoto wao.

2. Kuwakuza watoto katika jinsia zote.

Wazazi ndio shule ya kwanza kwa watoto. Watoto hujifunza kutoka kwa wazazi maana na majukumu ya baba na mama (au mme na mke).
Hivyo, baba anapaswa kuwa mfano mzuri wa kuigwa kwa watoto wa kiume, na mama kuwa mfano mzuri wa kigwa kwa mtoto wa kike kupitia maisha yao ya kila siku.

Ikiwa kama ni vigumu kwa mzazi mmoja kushiriki katika malezi, mtoto wa jinsia husika atengewa mazingira yatakayomwezesha kuiga na kuishi kadiri ya jinsia yake. Kwa mfano, kupata nafasi ya kuona jinsi familia za jirani zinavyoishi.

3. Kutomkaripia mtoto vikali kutokana na tabia yake.

Wazazi na walezi wananapaswa kuwa makini pale wanapowaonya watoto wao kwa kuwa wameonyesha tabia au mienendo hatarishi. Kwa mfano, kutompiga vikali mvulana kwa kuwa anajiremba au kuiga sauti za wasichana.
Makaripio makali huwafanya watoto kukubuhu na kujenga kiburi, na hivyo kuamua kuendeleza tabia husika.

Wazazi na walezi wanapaswa kujua ya kwamba watoto, hususani wakati wa balehe au kuvumja ungo, ni watundu sana na hupenda kuiga kila kitu. Hivyo, wazazi na walezi wanapaswa kuwa na upole huku wakiwafundisha madhara ya tabia hatarishi.

4. Kutoa fursa sawa kwa jinsia zote za watoto.

Watoto huwa njiapanda nyingi hususani wakati wa balehe au kuvunja ungo. Baadhi ya watoto huona ya kwamba jinsia tofauti na yao inapata faida sana. Hivyo huanza kuiga mitindo yao ya maisha, mingi ya mitindo hiyo ikiwa ni hatarishi.

Kwa mfano, watoto wa kike huona watoto wa wakipewa uhuru wa kwenda watakapo, kutopangiwa majukumu au kazi nyingi za kifamilia n.k. Hivyo, wasichana hao huiga mienendo ya kiume ili kujiridhisha. Tabia hii ikiachwa huwafanya wasichana hao kujihususisha kimapenzi na wasichana wenzao. Wazazi na walezi wanapaswa kutoa fursa sawa kwa wote ili watoto wote wafurahie jinsia zao tangu awali.

5. Kuwalea watoto kwa misingi ya dini.

Wazazi na walezi wanapaswa kuwalea watoto kwa misingi ya imani zao. Ili kufanikisha hilo, wazazi na walezi wanapaswa kuishi kandiri ya imani zao ya kila siku.
Malezi ya kidini huwafanya watoto kuona muhimu wao kwa mujibu wa jinsia zao.

Kwa mfano, wazazi kuwasimulia watoto habari za watu maarufu waliomtumikia Mungu katika dini husika kwa jinsia. Pia kuwaambia watoto ya kwamba Mungu alimuumba mtu mke na mtu mme ili wamtumikie.

6. Kuwalea watoto kwa mujibu wa jinsia zao.

Mtoto wa kiume anapaswa kulelewa kama mtoto wa kiume ili aweze kuwa mwanaume, na mtoto wa kike vivyo hivyo. Hata kama mtowazazi waliyoipendelea, mtoto aliyezali maadili mema na mwenendo unaokubalika.

Kwa mfano, ikiwa wazazi walipendelea mtoto wa kwanza awe wa kike, na akazaliwa mtoto wa kiume; wanapaswa kumlelea mtoto huyo kama wa kiume, na si kumdekeza. Watoto wengi wa kiume wanaodekezwa huwa mashoga.

Ikiwa kama wazazi na walezi (jamii kwa ujumla) watafanikiwa kuwalea watoto kwa misingi hiyo; kabla ya mtoto kuanza maisha tofauti na ya familia, kwa mfano kwenda shule ya kulala (bodi), changamoto ya mapenzi ya jinsia moja itakuwa imepunguzwa au kumalizika kabisa. Takwimu zinaonyesha kwamba watu wenye mahusiano ya jinsia huimarika wakiwa chini ya umri wa miaka 18.

Monday, July 16, 2012

MBINU ZA KUUKABILI USHIRIKINA

Ushirikina ni hali ya kuamini kuna haja ya kuwa na nguvu ya ziada kutoka kwa mtu au nafsi ili kuweza kufanikisha jambo fulani. Kwa mfano, kuamini kuna haja ya kufanya kafara (kuchinja na kumwaga damu ya mtu au mfugo) ili kuweza kupata kazi. Imani za ushirikina ni maarufu katika jamii na sehemu mbalimbali duniani.

Imani za ushirikina ni kukwazo kikubwa kwa jamii nyingi kwa kuwa:

Hupunguza nafasi za kusoma. Kuamini katika ushirikina kutochukua jitihada za kusoma ili kupata suluhu juu ya changamoto zinazoikabili jamii husika. Kwa mfano, kutegemea ushirikara kunaweza kuwazuia wafanyabiashara kutofanya tafiti mpya juu ya mwenendo wa biashara, hatimaye hufilisika.

Huongeza mzigo. Kuamini ushirikina kunamfanya mtu kuishi akiwa amevaa vitu mbalimbali ili kutimiza malengo, mfano, kuvaa irizi. Vitu hivyo kwa ujumla wake huongeza mzigo katika mwili wa mtu.

Huzuia malengo kutimia. Watu wanaoamini ushirikina huacha kufanya mambo waliyoyapanga kwa kuwa masharti hayaruhusu. Kwa mfano, mtu anayekwenda kufanya biashara fulani, akikutana na bundi asubuhi, kwa kuwa anaamini bundi ni ishara ya mkosi, mtu huyo hurudi nyumbani, hivyo, kuacha kufanya biashara kwa siku husika.

Huleta mfadhaiko. Ikiwa kama mtu anaamini irizi ndio kinga yake, kwa bahati mbaya akasahau kuvaa irizi siku fulani, siku hiyo ataishi kwa wasiwasi na hofu siku nzima. Au mtu akiamini mzee fulani ni mchawi, na akakutana nae, mtu huyo hupata mfadhaiko kwa kuogopa atakuwa amelogwa.

Huongeza changamoto za kimaisha. Kutokana na kuamini ushirikina, mshirikina hujinyima fursa nyingi za kusonga mbele. Kwa mfano, mtu anayeamini ya kwamba jirani yake ni mchawi, mtu huyo hukatisha mawasiliano na jiarani yake, pia, mtu huyo anaweza kuwaacha watoto wake bila ya uangalizi wowote kwa kuogopa wanawe watalogwa na jirani yake.

Mbinu za Kukabili Imani na Madhara ya Ishirikina.

Inawezekana kabisa kuepa ushirikina, na mtu husika asidhurike kwa kufanya yafuatayo:
Kutumia takwimu.
Ili kukwepa mawazo au uhusishwaji wa tukio fulani na imani za kishirikina, mtu anapaswa kusoma takwimu dalili n.kuhusu tukio husika. Kwa mfano, ili kutohusisha kifo na ushirikina, mtu anapaswakusoma takwimu kuhusiana na kifo cha mtu husika.

Kutafuta ushauri.
Ili kupunguza uwezekano wa madhara fulani kutokea mtu anapaswa kuomba na kufuata ushauri kutoka kwa wataalamu. Kwa mfano, ili kukwepa hasara katika biashara, mfanyabiashara anapaswa kutafuta na kutekeleza ushauri kutoka kwa wataalamu wa biashara kabla na wakati wa biashara husika.

Kujaribu nguvu ya ushirikina.
Ikiwa kama mtu anaamini ya kwamba bila ya kuwa na irizi hawezi kufanya vizuri katika mchezo, mtu huyo afanye maandalizi sahihi huku akiwa na imani ya kuwa atafanikiwa bila ya kukumia kizizi. Pia mtu huyo anaangalie kama mara zote anazotumia irizi je anakiwa? Kama kizizi ndio suluhu ya kufanikiwa, je kuna haja gani ya kufanya mazoezi?

Kumwamini Mwenyezi Mungu.
Kila kitu (kinachoonekana au kisichoonekana) kimeumbwa na Mungu. Mungu ndiye mtawala wa kila kitu. Ikiwa kama Mwenyezi Mungu ameweza kuumba kila kitu, je atashindwaje kushinda hila za ushirikina?

Ikiwa kama mambo hayaendi kama mtu alivyopanga, haimaanishi ya kwamba Mungu ameshindwa, bali kwa namna moja au nyingine Mungu anatoa somo. Kwani kutokana na matatizo yanayomkabili mtu, ndipo watu huamini na kutii uwepo wa Mungu. Kupiga magoti kwa Mungu na kufanya kazi kwa bidii ndiko kunakoleta suluhu ya kudumu.

Achilia mbali mila na tamaduni, imani za ushirikina zinachukua nafasi kubwa katika jamii kwa kuwa watu hawana suluhu dhidi ya changamoto zinazowakabili. Kwa mfano, kukosekana kwa elimu na tiba juu ya ugonjwa fulani unaosababisha vifo vingi, huwafanya watu katika jamii husika kuhusisha ugonjwa huo moja kwa na imani za ushirikina.

Monday, July 9, 2012

MBINU ZA KUPUNGUZA MAKALI YA MAJANGA

Hakuna mtu yeyote mwenye kinga dhidi ya janga lolote lile! Majanga huwakabili watu bila ya kubagua na mtu anapaswa kuyakabili bila ya kusita. Takribani mara zote majanga husababishwa na mahusiano ya kimapenzi, kazi, mabadiliko ya kiuchumi, ajali, mabadiliko ya afya n.k

Kiasi cha ukubwa wa janga au madhara yatokanayo hutofautiana sana; kikubwa ni kwamba kuna tofauti kubwa sana juu ya hisia na mbinu za kukabili janga husika. Kuna watu huwa na hisia chanya katika kuyakabili majanga (wanaamini watashinda), huku wengine husita, hukumbwa na hofu hatimaye hushindwa.

Ili kuweza kukabili janga na kuweza kupunguza ukubwa wa madhara, zifuatazo ni baadhi ya mbinu za kufahamu na kumudu:

a) Kuamini janga halikwepeki.

Kila mtu anapaswa kujua na kukiri ya kwamba kukumbana na changamoto tete katika maisha ni sehemu ya mapito ya kiumbe hai yeyote yule, hususani binadamu. Ikiwa kama mtu amekumbwa na hali ngumu anapaswa kujua kuna wengine wenye hali ngumu zaidi.

Kwa mfano, kama mtu amesalitiwa au kuibiwa mali zake anapaswa kujua ya kwamba kuna watu walio chini ya uangalizi wa daktari (ICU) ili kunusuru maisha yao au kuna familia zisizo na makazi wala chakula kutokana na mafuriko au maporomoko ya ardhi.

b) Kutolazimisha suluhu ya haraka.

Janga fulani linapotokea watu hufanya jitihada ili kuweka hali sawa ndani ya muda mfupi au haraka iwezekanavyo. Haishauriwi kusisitiza suluhu ya haraka, kwani takribani suluhu nyingi za haraka, zinazodhaniwa kuwa ni za kudumu hutuliza maumivu tu na hivyo kuongeza ukubwa wa tatizo nyakati za usoni. Suluhu nyingi za haraka hazina umakini.

Kwa mfano, kama mtu amesalitiwa kimapenzi, na akaamua kuanzisha mahusiano mapya ndani ya muda mfupi, mahusiano hayo mapya huleta madhara makubwa au kiafya au kiuchumi isivyotarajiwa.

c) Kutolaumu historia.

Muda mfupi baada ya adha fulani kutokea, watu wengi hujilaumu wenyewe au watu wengine kwa uzembe uliofanyika. Watu wengi husema "ningejua...ninge... Kauli kama hizo hazisaidii kitu chochote katika kuleta suluhu.

Hali kama hiyo huzuiowa kwa kubadili mawazo; kwa kuamini ukweli kwamba hakuna binadamu aliyekamilika, pia watu werevu hujifunza kutoakana na makosa wa wenzao, ikiwa makosa hatafanyika, kujifunza kutafanyikaje? Majanga hutumika kama kutoa somo kwa siku zijazo.

d) Kuangalia manufaa ya tukio.

Japokuwa majanga yote ni machungu,pia katika uchungu huo kuna chembechembe ndogo sana za utamu. Chembe hizo ndogo hugundulika baada ya kuchambua mkasa kuanzia mwanzo mpaka mwisho. Baada ya uchambuzi wa kina, mhanga anaweza kujua uimara na udhaifu wake. Majanga huwa ni kipimo kuzuri dhidi ya mahusiano ya mhanga na jamaa zake wa karibu.

Kwa mfano, baada ya kufilisika kiuchumi, mhanga anaweza kujua nani ni rafiki, ndugu au jamaa wa kweli; kwani undugu ni kufaana na siyo kufanana. Majanga hutoa somo kwa watu wengine juu ya mienendo ya watu wao wa karibu.

e) Kuamini suluhu itapatikana.

Kama inavyosemwa, hakuna kinachodumu milele, kila kitu kitapita, hivyo basi, mhanga anapaswa kuamini ya kwamba hata machungu aliyonayo yatapita.
Uzoefu unaonyesha ya kwamba, majanga hutisha sana siku za mwanzo, baada ya muda fulani mhanga hupata ahueni na hatimaye, kutokana na juhudi, suluhu ya kudumu hupatikana. Kwa mfano, wakati wa ajali kabla ya huduma ya kwanza hali ni mbaya ikilinganishwa na wakati baada huduma ya daktari.

f) Kuepuka mjumuisho.

Janga huathiri sehemu fulani tu ya maisha ya mtu. Kupata msukosuko katika sehemu A ya maisha haimaanishi ya kwamba sehemu B nayo itapata msukosuko na kushindwa kufanya kazi.

Kwa mfano, mtu anapoenguliwa kazini huku familia yake na ndugu zake wakimtegemea, haimaanishi kwamba mrafiki na jamaa wengine watamsaliti; kwani watu hao hutoa ushirikiano (hutoa misaada au kutafuta kazi) ili kuhakikisha maisha yanasonga mbele. Hivyo haipaswi kuona ya kwamba janga fulani litafunga milango mingine.

Monday, July 2, 2012

MBINU ZA KUEPUKA TAMAA MBAYA

Tamaa mbaya ni hali ya kutaka kumiliki mali zaidi ya mahitaji halisi; hali ya mtu kutotaka kuridhika, kwa mfano, kurudia rudia chakula ili hali watu wengine wanakosa. Tasnia ya matangazo hutumia mwanya huu kwa kutoa matangazo bora yanayoteka akili za watu na kuwaamuru watu wagombanie bidhaa ili wapate furaha, kwa lengo la kuvutia wateja.

Yafuatayo ni madhara ya tamaa mbaya:

¤ Kukosa kujitawala. Watu wenye tamaa mbaya hawawezi kumiliki hisia zao, hawawezi kutawala malengo yao; huyumbishwa na pepo za ushindani.
¤ Kushindwa kuweka malengo. Watu wenye tamaa mbaya hawawezi kuweka kipimo halisi cha malengo yao, wengi huvutwa na malengo au mipango ya wenzao ili wapate kuwashinda.
¤ Kuingia kwenye madeni. Kutaka kujilimbikizia mali kunawafanya watu kukopa kwa pupa na kulipia mambo yasiyo na tija ya kweli kwao. Madeni hayo hupelekea mtu kudhalilika na kufilisiwa baada ya kushindwa kulipa.

¤ Kukiuka maadili. Tamaa zilizopitiliza huongeza uwezekano wa mtu kukiuka miiko ya kazi au maadili ya jamii yake kama vile; udanganyifu, wizi, utapeli n.k
¤ Kuvunja mahusiano ya mtu. Tamaa mbaya huleta mtafaruku hususani pale mtu anapoingilia na kuhatarisha maslahi ya mwenzie au jamii yake. Kwa mfano kusogeza mpaka wa shamba au kiwanja.
¤ Kuleta tabia hatarishi. Tamaa mbaya hupelekea tabia hatarishi kama kukosa usingizi, kukosa hamu ya kula, hasira n.k. Hali hizo hupelekea kupungua kwa kinga ya mwili na uzito na hatimaye magonjwa.

Jinsi ya Kukwepa Tamaa Mbaya

1. kukubali mafanikio. Mtu anapaswa kutizama ubora wa mali alizo nazo, ikilinganishwa na awali, bila ya kuangalia nani anamiliki nini. Kuridhia mafanikio ni silaha muhimu sana.

2. Kujitathimini na kuweka malengo. Mtu anapaswa kujiweka mbali na hisia mbaya; hisia za kukosa, na kujiangalia kwa kina mahitaji halisi. Mahitaji halisi huwekwa kulingana na uwezo wa mtu husika.

3. Kukwepa kujithaminisha na mtu.
Mtu asifadhaike kutokana na hatua za mafanikio jamaa zake walizopiga, kwani kila mtu anapata fursa tofauti tofauti na kwa nyakati tofauti. Pia kamwe mafanikio hayawezi kufanana, kwani mafanikioa ni kama vidole.

4. Kuwasaidia wengine. Kuwawazia na kuwasaidia watu wanaokosa mahitaji ya msingi kama chakula, makazi na mavazi husaidia kupunguza tamaa mbaya kwa kiasi kikubwa, hii ni ngumu sana kwa watu wenye wivu. Ni muhimu kuwasaidia yatima, wajane, wazee wasio na walezi, vilema n.k.
Katika shida na tamaabu zao.

5. Kumwomba Mungu.
Mtu anapaswa kumomba Mungu kadiri ya imani yake, kwani kila mtu anaamini Mungu yupo. Mtu anapaswa kumwomba Mungu ampatie afya, amani, utulivu wa akili na nafsi na mkate wa kila siku; kwani vitu hiyo ni bora kuliko kumiliki mali zenye thamani kubwa kama tani kadhaa za dhahabu.