Monday, September 26, 2011

UWAZAJI CHANYA

Je umewahi kujiuliza, kwa nini kuna hisia tofauti- tofauti juu ya janga fulani? Kwa nini majanga kama kupoteza ndugu, mafuriko, n,k upokewa kwa hisia tofauti na wahanga?

Hii ni kwa sababu watu hupokea na kuchambua taarifa kwa namna tofauti, wengine chanya na wengine hasi.

Watu wanaochukua majanga kwa mtazamo chanya wanafaida zifuatazo:
-huimarisha mahusiano yao na jamii inayowazunguka
-huongeza ufanisi katika taaluma, kazi n.k
-huimarisha kinga ya mwili
-hupunguza maumivu ya ajali na majeraha mengineyo

Je Mtu Anawezaje Kuwaza Chanya?

Kukataa mawazo hasi ni hatua muhimu na ya awali kwa mtu yeyote anayetaka kuwa na furaha na ustawi maishani.
Uwaji chanya unafaa uwe wa kudumu, na si wakati wa matatizo au baada ya ushauri kutoka kwa wanasaikolojia na wataalamu wa akili.

Ili kuwaza chanya, yafuatayo yanapaswa kuzingatiwa kipindi chote cha maisha ya binadamu.

1) Uwazaji chanya juu ya mtu binafsi.
Epuka kuishi kwa kujilinganisha na watu maarufu kwenye TV, jamii n.k.

Kipimo cha mafanikio kiwe ni malengo na si mafanikio ya wale uliozaliwa nao, uliosoma nao, uloanza nao kazi n.k.
Yakubali mapungufu yako, na dhamiria ili hayo mapungufu yasitokee tena maishani.

2) Kuwaza chanya juu ya yaliyopita.
Historia haibadilishwi, ikubali hata kama ina chembechembe nyingi za uchungu.
Kuilaumu historia kana kwamba ndiyo iliyopelekea hali ngumu uliyo nayo haisaidii chochote!!
Mfano, kama baba angenipeleka shule...., kama fulani asingenisaliti... n.k

Kumbuka yote mazuri yaliyotokea nyuma, yatakusaidia na kukupa ujasiri wa kufanya maamuzi.
Kwa mfano, wazazi wamenipa malezi bora, kusalitiwa kumeniimarisha n.k
Kumbuka mawazo, mitizamo na mawaidha ya wazazi, marafiki n.k ingawaje hawapo duniani.

3) Kuwaza chanya juu ya yajayo.
Kesho inatengenezwa na mitizamo yako ya leo. Ukiwaza kwa ujasiri na kijiamini kuhusu kesho kunaongeza uwezekano wa kufanikiwa.

Hata kama changamoto zitatokea utaweza kuzikabali, kuwa na mipango sahihi bila ya malalamiko na hasira.
Mfano, nimefeli mtihani! Akili imefunguka na ntasomea ufundi kisha kujiajiri binafsi.

4) Kuwaza chanya juu ya watu na mazingira.
Kumbuka hakuna kilichotimilifu, ila kuna mema na matamu katika kila mtu na mazingira.

Usijenge hasira juu ya watu na mazingira fulani, amini watu na mazingira huku ukifanya jtihada kukabiliana na changamoto.

Jitahidi kuelewa kwa undani watu na mazingira husika.
Jiulize je, ni watu wote walio katika mazingaira fulani (mfano mijini) wamefanikiwa?

Jenga imani na wote wanaokuzunguka (marafiki, ndugu, majirani n.k) na kuchukua mawazo na changamoto wanazotoa kama mtaji kwako. Na hatiamye.

5) Mshirikishe Mungu.
Jaza moyo wako mawazo ya kiimani kwa kumtanguliza Mungu, kwani dini (imani) zote zinajenga utulivu wa akili.
Amini ya kwamba kufanikiwa ni kwa ajili ya binadamu wote, watu wote ni sawa mbele ya Mungu. Mruhusu Mungu akupe silaha na nguvu za kupambana na hila zote kutoka kwa waovu.

No comments:

Post a Comment