Monday, March 26, 2012

JE PESA NI KILA KITU?

Je ili kupata takribani kila kitu mtu anachotaka, ianampasa mtu kuwa na pesa? Jibu ni NDIO, na hiyo ndio sababu inayowafanya watu watafute pesa kila wakati; iwe usiku au mchana. Watu wamepewa majina mengi kama; mafisadi, wezi wa kalamu, matapeli, n.k kutokana na harakati zao za kusaka pesa. Huku pesa ikipewa majina kama; mkwanja, mapene, mawe, noti...

Kutafuta na kumiliki pesa nyingi ndi
o lengo la watu wengi. Hii haibadili ukweli kwamba watu hawapati pesa za kutosha kukidhi mahitaji yao; hata ya kila siku. Ikiwa pesa hazitoshi, je ni lazima kutafuta pesa?

Ukiwaza kwa kina utagundua kwamba, hakuna binadamu anayetaka pesa. Watu wanataka bidhaa au huduma, na wala si pesa. Hivyo, watu wanatafuta pesa ili kununua bidhaa au huduma kwa ajili ya kukidhi mahitaji; ili kukidhi mahitaji yasiyokwisha.

Kuelekeza mawazo na jitihada nyingi katika kutafuta pesa kumewafanya watu wasitafute njia mbadala za kukidhi mahitaji yao. Watu wanaamini pesa ndio kila kitu, hata wanasahau sababu za kutafuta pesa. Kuna baadhi ya watu wanatafuta pesa ili kuwa na 'usalama' na furaha, vitu ambavyo haviitaji pesa.

Kutaka pesa nyingi kumewafanya watu kuwa watumwa wa pesa, kumewafanya watu wachague au waache fani zao za awali na kukimbilia kwenye fani zenye uhakika wa pesa nyingi ili kununua furaha, bila ya kujali hatari (athari) zinazohusiana na fani husika.

Takribani watu wote maarufu na waliofanikiwa walielekeza nguvu zao kulinganana na vionjo (hobby) vyao, na wala si kufuta wingi wa fedha. Waliboresha vipaji vyao, na vipaji vyao viakawaletea pesa, heshima, furaha na usalama.

Ikiwa mtu anataka kupata mafanikio maishani, anapaswa kujiuliza; JE NINAHITAJI NINI HASA?
Ili kujibu swali hilo, mtu anapaswa kuandika vitu vyote anavyotaka kufanya au kuwa navyo bila ya kujali gharama. Wakati huo mtu husika akiwa mkweli dhidi ya nafsi yake; juu ya uhitaji wa bidhaa au huduma husika. Kisha mtu apitie tena orodha yake kwa kina huku akikadiria gharama.

Kwa kufanya hivyo kutamfanya mtu kutosema 'nahitaji maisha bora', bali atakuwa na malengo mahususi; kama nahitaji gari aina..., nahitaji nyumba iliyo na..., nahitaji elimu ya... n.k. Mtu atakuwa na malego ambayo, kama akielekeza nguvu ipasavyo, atakuwa na 'maisha bora'.

Kuwa malengo mahususi kunamfanya mtu kujua kiasi gani cha pesa anachohitaji, pia kujua mbinu mbadala anazohitaji ili kutimiza lengo husika.
Mbinu mbadala kwa kila jambo ni muhimu sana, kwani kuna baadhi ya mambo hayahitaji pesa, bali ufahamu, ushauri..... ambao unaletwa na mahusiano mazuri baina ya mtu na jamii yake.

No comments:

Post a Comment