Monday, March 5, 2012

JINSI YA KUBANA MATUMIZI

Ubora wa matangazo, tabia ya mtu na kuwepo kwa bidhaa ndizo sababu zinazopelekea kuwepo kwa 'ulafi' nyakati hizi, hususani maeneo ya mijini.

Je kuwepo kwa bidhaa na huduma kwa wingi hupelekea furaha? Jibu ni HAPANA. Chunguzi zilizofanywa miongoni mwa vijana waishio miji mingi duniani, ikilinganishwa na wazee wao ambao hawakua na uwezo wa kumudu matumizi, zinaonyesha kwamba vijana wanayo furaha ndogo.

Je Jamii Itapata Faida Gani Ikiwa Itapunguza Matumizi?

1. Uhifadhi wa rasilimali. Rasilimali asilia zitatunzwa kwa kizazi kijacho ikiwa kutakuwa na matumizi endelevu ya huduma na bidhaa zitokanazo.
2. Mazingira safi. Uchafu utapunguzwa ikiwa kama kila mtu atatumia bidhaa na huduma kwa uangalifu.
3. Kukwepa mzigo wa madeni. Haitakuwa lazima kuchukua mkopo kila mara ili kugharamia matumizi ya kawaida. Hivyo, kupunguza utegemezi wa kifedha.
4. Kurahisisha maisha. Matumizi sahihi humfanya mtu ayaone maisha ni rahisi. Hivyo, kupunguza dhana ya maisha ni magumu katika fikra.

Mikakati ya Kupunguza Matumizi.

1. Kuweka vipaumbele.
Mtu anapaswa kuweka vipaumbele kulingana na matumizi ya fani, masomo, burudani n.k si kuyumbishwa na makundi. Vipaumbele viwekwe kwenye orodha kulingana na umuhimu wake.

2. Kuchambua matumizi.
Mtu anapaswa kufanya uchambuzi wa kina juu ya mahitaji ya wakati husika. Uchambuzi unaweza kufanywa kwa kujiuliza maswali kama; je ni lazima kununua bidhaa husika? Je hakuna mbadala wa bidhaa husika? Je kama nisingekuwa na fedha? n.k.

3. Kuwafikiria wengine.
Ni bora kununua bidhaa na huduma ambazo si tu zitamsaidia mnunuaji bali pia jamii ya wahitaji inayomzunguka kama; yatima, wajane, wazee, fukara n.k wanaomzunguka.

4. Kuepuka majina ya makampuni.
Yapasa kufanya uchambuzi kuhusu ubora na gharama, na si kununua bidhaa kwa kuwa imetengenezwa na kampuni fulani. Baadhi ya makampuni makubwa hutengeneza bidhaa hata zilizo chini ya kiwango, lakini hupata manunuzi makubwa kwa kuwa hufanikiwa kutangaza, kutoa punguzo la bei n.k

5. Kuahirisha matumizi.
Ni bora kusitisha ununuzi wa bidhaa au huduma isiyo na ulazima kwa siku, wiki au miezi kadhaa. Kusitisha manunuzi husaidia kufanya tafiti juu ya soko pia, husaidia kupunguza hamasa au ushabiki katika matumizi

6. Kupunguza matumizi ya kadi.
Mageuzi ya teknolojia yamewezesha watu kuwa karibu zaidi na fedha zinazohifadhiwa benki. Pia teknolojia imewezesha kufanya manunuzi kwa kutumia kadi za ATM.
Pia inashauriwa, kupunguza kiwango cha fedha za tahadhari mtu anazokuwa nazo popote aendapo.

7. Kuwalinda watoto.
Watoto ni sehemu kubwa sana ya jamii. Hivyo wanapaswa kusaidiwa kupunguza matumizi kwa:

(a) Kupunguza matumizi ya TV. Matangazo yanayoonekana kwenye TV huteka hisia za watoto. Hivyo, kuwafanya wanunue bidhaa hata bila ya wazazi/ walezi wao kujua.
(b) Kueleza ubaya wa matangazo. Watoto waelezwe ubaya wa kununua bidhaa kutokana na ushawishi wa matangazo.
MATUMIZI BILA AKIBA, FEDHA ZITATUKIMBIA..

No comments:

Post a Comment