Monday, April 30, 2012

MBINU ZA KUKUZA MAHUSIANO BAINA YA WATU

Mahusiano baina ya mtu na jamii yake ndiyo yanayomfanya mtu au afanikiwe au asifikiwe. Mahusiano baina ya mtu na mtu hutegemea uwezo wa mtu husika kushirikiana na jamii yake, kushikiana kunakojengwa na kutegemeana; na si kutegemea.

Ili kuboresha mahusiano, yafuatayo yanapaswa kuzingatiwa:-

a) Upendo.
Ili mtu apendwe anapaswa kujipenda kwanza; kujipenda huanza kwa muonekano wa ndani na kisha wa nje. Kujipenda na kuwapenda watu wengine huonekana machoni mwa watu kupitia mienendo. Mtu anayewapenda wenzake hujitahidi kutoa msaada wa hali au mali ili wenzake watimize malengo yao.

b) Kukumbuka majina.
Mtu anapowaja watu anaowasiliana nao kwa majina. Au kuwaeleza jinsi anavyojua kule watokako huwatia watu faraja, kuwafanya wote wajione ni jamii moja. Pia huwafanya watu husika kujiona ni muhimu (wana thamiwa) miongoni mwa jamii.

c) Kukubali juhudi za watu.
Kukubali matunda (matokeo) ya kazi za watu wengine; kwa kuzipa thamani au ubora unaotakiwa hudhihirisha harakati za watu na kuwafanya waongeze matumaini na juhudi.

d) Kusikiliza kwa makini.
Kusikiliza ni bora zaidi ya kuongea katika nyakati nyingi. Mtu hudhihirisha jinsi gani habari yake inavyoungwa mkono kwa kadiri anavyosikilizwa. Hivyo kukuza hekima na uelewa wa msikilizaji. Baada ya kusiliza, mtu anapaswa kujibu kadiri ya busara na dhamira yake.

e) Kuruhusu hisia za watu.
Kuruhusu hisia, mtizamo, au mada kutoka kwa mtu/watu zijadiliwe humfanya mtu/watu kuzungumza kwa uhuru juu ya kufanikiwa na changamoto zao. Hivyo kumfanya mtu/ watu kufurahia uhusiano wao na jamii yao.

f) Kutia moyo.
Kuwatia moyo watu ambao hawakufanikiwa kiasi cha kuridhisha hutoa ahueni kwa mhanga. Yafaa kuwatendea watu kadiri ya mtu anavyotaka atendewe na wenzake. Kuwatakia watu heri husaidia kuepuka mawazo au kauli za kuwarudisha nyuma.

No comments:

Post a Comment