Monday, December 19, 2011

KUSIKILIZA KWA MAKINI

Kufanikiwa au kutofanikiwa kunafanikishwa na ubora wa mawasiliano. Mawasiliano bora humwezesha mtu kueleweka na kukubalika. Mawasiliano ni muhimu kwa mahusiano baina ya; mtu na nafsi, mtu na mtu, mtu na familia, mtu na marafiki n.k

Maneno tunayozungumza na kusikia hupelekea; faraja au huzuni, usalama au hatari, kukubalika au kukalika n.k. Mbali na maneno, ujumbe wa ishara (kama vile kutazama, tabasamu, kuchezeha kichwa, matumizi ya mikono n.k) unamadhara makubwa sana au sawa na maneno/sauti.

KUSIKILIZA KWA UFASAHA.

Jambo moja na la muhimu katika mawasiliano ya sauti ni KUSILIZA. Binadamu amepewa mdomo mmoja na masikio mawili ili.......... Umakini katika kusikiliza hukuza na kuboresha mawasiliano, humsisimua mzungumzaji na kumhamasisha msikilizaji.

Kufanikisha usikivu fasaha; yafuatayo ni muhimu:
1) Kufahamu lugha ya ishara.
Kuwa makini na matumizi ya viungo vya mwili vya mzungumzaji; kama vile mikono, miguu, kichwa, tabasamu n.k. Lugha ya ishara hutumiwa na mzungumzaji kuboresha ujumbe anaotoa na hivyo kuboresha mawasiliano.

2) Kuondoa vikwazo.
Ili kusikiliza kwa ufasaha, mtu ajitahidi kadiri ya nguvu zake zote kuondoa mawazo na changamoto zinazomsonga. Vikwazo vinaweza kuwa kelele, mtazamo hasi juu ya ujumbe n.k. Kuondoa vikwazo kunawezeshwa na kuelekeza mawazo pia kujenga taswira juu ya kinachozungumzwa.

3) Kuomba ufafanuzi.
Kama mtu hajaelewa ipasavyo; kama anao wasiwasi au kama hajaelewa baadhi ya maneno n.k; anapswa kuomba ufafanuzi. Komba ufafanizi kuwe kwa lugha ya upole na unyenyekevu, lugha ya ukali kama vile "kwani hauna sauti? "unaniongelea kama mgonjwa?", "mimi sikusikii" n.k huondoa hari ya mzungumzaji; na hivyo kusitisha mazungumzo.

4) Kuthibitisha ulichosikia.
Mawasiliano yoyote hutegemea mwitikio. Ili kuhakikisha kuna uelewano hususani mambo ya msingi; inampasa msikilizaji kuthibitisha alichosikia na kuelewa, anapaswa kutoa mrejesho kwa mzungumzaji.
Mrejesho unaweza kuwa ni ufupisho wa ujumbe au ufafanuzi kwa kadiri ya alivyoelewa. Mfano, Mzungumzaji: nitafute kesho saa moja.
Msikilizaji: nikutafute kesho saa moja ya asubuhi?

5) Kutambua hisia za mzungumzaji.
Hisia au hali aliyonayo mzungumzaji husaidia kujua aina ya ujumbe anaoutoa. Mtu anapaswa kujua sababu za mzungumzaji kuongea kwa lugha ya ukali, lugha ya upole, kuangalia chini au pembeni, kuongea mfululizo n.k. Kujua hisia husaidia kuchukua hatua sahihi ili kuelewa ujumbe.
BINADAMU AMEPEWA MDOMO MMOJA NA MASKIO MAWILI ILI, ASIKILIZE ZAIDI YA KUZUNGUMZA.

No comments:

Post a Comment