Monday, December 12, 2011

UBUNIFU.....unaendelea.

Hatua Tatu za Kuongeza Ubunifu.
1) Kuamini inawezekana.
Kuamini jambo unaloona ni gumu; ya kwamba linawezekana huweka akili katika mwendo (njia) kuelekea kwenye suluhu. Kuamini huimarisha misingi na mazingira kuelekea "kusadikika".

Mtu anapaswa kuamini katika vitu vinavyoonekana ni vidogo na havina msaada kwa kuwa, siri za mafanikio hazitegemei mambo makubwa na maajabu ili kufanikiwa.

2) Kuondoa neno "HAIWEZEKANI" katika matamshi.
Mtu anaposema sentensi fulani juu ya jambo fulani mara kwa mara, uhalisia wa anayosema hujitokeza katika matendo.
Pale mtu anapotamka jambo fulani haliwezekani kabisa au zaidi ya ubora fulani, huifanya akili kutochukua hatua zozote au za ziada.
Wataalamu wa akili wanasema, analosema mtu ni matokeo ya mawazo yake, na kwa kiasi kikubwa humtokea. Waswahili wanasema, mdomo huumba.

3) Kukubali kupokea mawzo mapya.
Kufungua akili na kukubali kupokea mawazo mapya ni kama kuongeza mbolea na maji kwenye mimea.
Mtu anapaswa kuchambua mawazo mapya kwa kina, na kwa kadiri ya mahitaji, kudadisi ni kwa nini na kwa vipi mawazo husika hufanya kazi.

Jinsi Gani ya Kuishi mbinu za Ubunifu?
1) Kutenga muda na eneo tulivu kwa ajili ya tathmini ya kila siku, kabla na baada ya kulala.
2) Kujenga mazoea ya kutumia akili kuliko nguvu katika kukabili changamoto.
3) Kujenga mazoea ya kuishi kwa kufuata mawazo mapya na si kuishi kwa mazoea.
4) Kufanya kazi na mazoezi ambayo huimarisha na kukuza seli za akili. Mfano, michezo ya kompyuta.
5) Kukuza vionjo na silika; kuacha kushangaa bali kufanya jitihada ili kinachoonekana au kuwazwa kitimie.

Pia mtu anapaswa kufahamu ya kwamba:
¤ Kipawa asilia hakiletwi na milango mitano ya fahamu tu, bali akili fichika (subconsious mind).
¤ Akili fichika inafanikisha ujenzi wa taswira ambayo hupokewa na milango ya fahamu ili kufanikisha ukweli.
¤ Ubunifu wote huletwa na akili fichika.
¤ Ubunifu huonekana baada ya kuweka misingi na kuwaza chanya juu ya maisha.

No comments:

Post a Comment