Monday, December 5, 2011

UBUNIFU

Ubunifu ni nguvu mtu anayoibua kutoka katika taswira, taswira ya kitu kinachoonekana. Ubunifu ni bora kuliko kuwa na maarifa kwani, maarifa yana kikomo ili hali ubunifu hutapakaa ulimwenguni kote, huchochea mabadiliko yanayozaa maendeleo.

Ubunifu ni kiunganishi kati ya kipawa alichonacho mtu na mchango ulimwengu unaotoa kwa mtu husika. Kila kinachoonekana na taswira yake huwekwa katika akili, baada ya muda hutekelezeka kupitia ubunifu.

Kuna aina kuu mbili za ubunifu, nazo ni;
1) Ubunifu sanisi.
Katika aina hii ya ubunifu; mawazo, fikra na mipango aliyonayo mtu hupangwa katika mfumo mpya na tofauti. Aina hii hutegemea elimu na uzoefu alionao mtuu juu ya fani fulani.

2) Ubunifu kipaji.
Aina hii huvuta hisia na maono pamoja, hujengwa na jinsi mtu anavyopokea na kujibu yale anayoambiwa na mazingira. Ubunifu huu hautegemei uzoefu alionao mtu, bali elimu kidogo juu ya nyanja fulani. Ubunifu huu ndio chanzo cha ugunduzi.

Jinsi ya Kijenga Ubunifu.

1) Kuchangamsha akili kwa kusoma.
Kusoma ndio njia ya kuaminika yenye kukuza vipawa na siri zilizofichika katika katika dunia.
Mtu anapaswa kusoma yale yanayonfanya afikiri kwa kina, yanayotoa changamoto juu ya imani ya mtu na kuonyesha njia fasaha ya kufuata. Kumbuka siri za dunia zimefichwa kwenye maandishi.

2) Kuendeleza maboresho.
Kila umbo la kitu kinachoonekana ni maboresho yatokanayo na taswira, taswira aliyokuwa nayo mtu kichwani juu ya umbo hilo.

Uendelezwaji wa maboresho unawezeshwa na mbinu sahihi za kupumzisha akili na mwili. Kila siku mtu ahakikishe anapata mahali kwa ajili ya kupumzika; mahali ambapo atakaa kimya; kufunga macho na kupumua huku akifikiri juu ya mwenendo wa siku inayoisha, inayofuata na maisha kwa ujumla.

3) Kuwa na lengo.
Mtu anapaswa kuwa na lengo pamoja na azma juu ya maisha yake; juu ya maisha ayatakayo.
Ili kufanya hivyo, mtu anapaswa kuvunja vunja na kuunga upya vipande vianavyojenga lengo na azma husika. Kufanya huvyo husaidia kuona mapungufu na jinsi ya kuyakabili kabla au wakati wa utekelezaji wa lengo husika.

4) Kuwa na nguvu za umakini.
Nguvu za umakini huletwa na ridhaa na nidhamu ya mtu, ridhaa na nidhamu ya kutaka kutekeleza kile anachoamini ni sahihi kwa manufaa yake na ya jamii nzima. Nguvu za umakini huwezeshwa kwa utizamaji wa kina juu ya lengo, matendo, mienendo na hisia kuelekea ufanikishwaji wa azma husika.

5) Kumiliki vionjo.
Tamaa na jazba ni visafiria vianyotumiwa na wahujumu ili kuleta vikwazo; kukatisha tamaa; kuondoa imani; kujenga hofu na hatimaye kutochukua hatua sahihi. Hujuma hushambulia nafsi zaidi, hujuma zinaweza kupunguzwa na kuondoshwa kwa jitihada za mtu kumiliki mawazo yake, mienendo na mitizamo kwa hali ya juu.

Ubunifu uhamasishwa na tabia ya mtu ya kufikiri na kudadisi juu ya njia mbadala na sahihi ili kupata suluhu rahisi katika kutatua changamoto inayomkabili mtu binafsi na jamii kwa ujumla

No comments:

Post a Comment