Monday, June 4, 2012

MBINU ZA KUWINDA AJIRA (1)

Changamoto ya ukosefu wa ajira ni kubwa, si kwa Tanzania tu bali hata kwa mataifa mengine. Takribani kila Taifa kuna idadi kubwa ya watu wanaopunguzwa kazini kutokana na mabadiliko ya teknolojia au ili kumudu gharama za uendeshaji, pia kuna wahitimu wengi kutoka vyuoni.

Hatari kubwa ni kwa wahitimu kutoka vyuoni kwa kuwa waajiri mengi humtaka mwajiriwa mtarajiwa awe na uzoefu wa miaka kadhaa katika kazi anayotaka kuomba.
Hivyo wahitimu wanapaswa kufanya kazi ya ziada kwani santuli (CV) zao hazina thamani, zote zinafanana.

Kutokana na kufanana kwa CV, mhitimu anapaswa kuhakikisha anajiuza, si kutegemea CV impatie kazi.
Mtihitimu anaweza kuijuza kupitia: (i) muonekano wake (ii) vionjo alivyo navyo (iii) hamasa na (iv) imani aliyo nayo juu ya kufanikiwa. Pia mtu anapaswa kuishi kadiri ya fani yake kama: kuvaa mavazi ya heshima, kuongea kwa ufasaha, kutekeleza majukumu (kuacha uvivu) n.k. Vitu hivyo ni bora zaidi ya elimu ya darasani.

2.0. MIKAKATI

2.1. Kuwa na Lengo.
Soko la ajira ni ngumu, pia linabadilika badilika kila wakati. Watu wanaohitaji kazi ni wengi kuliko nafasi zinazotolewa na soko la ajira.

Hivyo mtu yeyote anayetafuta kazi lazima awe na LENGO mahususi. Watu wengi, hata wasomi wa vyuo vikuu hawana malengo. Wahitimu wengi huwa wamejiandaa kitaaluma tu! Hawajiandai ili kupata misingi ya kukabiliana na changamoto maishani. Hivyo kupata changamoto nyingi katika kujikwamua kimaisha.

Katika mchakato mzima wa kazi, kuna makundi matatu ya watu; washindi, washindi wasiojitambua na wasiojitambua.

i) Washindi.
Watu hawa hupata kazi wanayoitaka, kipato wanachotaka na kufanya kazi katika mazingira wanayotaka. Watu hawa ni majasiri (hujiamini), hutumia rasilimali zao kwa makini, wapo tayari kumfuata mtu mwenye madaraka (mf Mkurugenzi) yeyote na kumweleza malengo na changamoto zao. Watu hawa nui wachache sana.

ii) Washindi wasiojitambua.
Watu hawa wana dhamira ya dhati ya kupata na kufanya kazi, wanatumia jitihada zao, wanajiamini kidogo (ni waoga), hutegemea kupata kazi zinazotangazwa magazetini n.k. Huwa hawapati kazi kwa haraka kwa kuwa hawapo tayari kusimamia malengo yao, pia hawaelekezi nguvu zao kwa makini.

iii) Wasiojitambua.
Watu hawa hawajui ya kwamba hawajui, yawezekana wamesoma, lakini hawajitambui; elimu yao hijawakomboa. Huwa wanaishi bora mradi wakiamini kupata kazi ni bahati, na bahati yao haijaifika. Ni waoga kupindukia. Humtegemea Mungu kwa kila jambo hata kwa mambo yaliyo ndani ya uwezo wao.
KUPATA KAZI KUNATAKA KUFAHAMIKA ZAIDI YA KUWA NA UWEZO WA DARASANI. Itaendelea......

No comments:

Post a Comment