Monday, June 18, 2012

MBINU ZA KUWINDA AJIRA (3)

5. KUPATA AJIRA YA KUDUMU.
Ni vigumu kupata au kuwa na uhakika wa kupata ajira ya kudumu, hususani katika taasisi binafsi. Hata hivyo, kuna watu wachache waliomudu kuwa na uhakika wa kufanya kazi katika kampuni au taasisi husika kwa muda mrefu; hata kuwa mtu muhimu sana katika eneo la kazi.

Ili kuwa na uhakika wa kufanya kazi kwa muda mrefu, mtu husika anapaswa:

(a) Kujiendeleza katika fani husika.

Kujiendeleza kitaaluma ni muhimu sana. Kujiendeleza kunaweza kwa kuhudhuria semina, kusoma vitabu, kuhudhuria makongamano.
Watanzania wengi hawapo tayari kulipia gharama zao binafsi ili kujiendeleza; hawapo tayari kununua na kusoma vitabu, kulipia na kuhudhuria makongamano au semina n.k. Hivyo hujikuta wakidumaza fani zao na utendaji kazi wao.

(b) Kujitolea

Kuna wakati mgumu katika maisha; wakati ambao mtu analazimika kutafuta kazi huku hajui aazie wapi.
Katika kipindi kama hicho mtu anapaswa kutafuta mahali atakapofanya kazi kwa muda kama mfanyakazi wa kuijtolea huku akipewa malipo kidogo kama nauli.
Kujitolea kufanya kazi kutamfanya mtu apate 'mitandao' ya ajira, kumwondolea msongo mawazo, kuongeza maarifa n.k. Kufanya hivyo kutamsaidia mtu kupata ajira ya kudumu kwa haraka.

(c) Kuunda mitandao

Watu wengi hupata kazi kutoka kwa watu wanaofahamiana nao. Kupata ajira kunahitaji kufahamika zaidi ya kuwa na uweledi katika fani husika.
Mtu anapaswa kuwa na kundi la marafiki katika nyanja tofauti tofauti za maisha, na marafiki wenye madaraka na ushawishi tofauti ambao watamuuunganisha na nafasi za ajira wakati wiowote anapotaka ajira.
Kutoka hatua moja kwenda nyingine kuna mlango. Mlango huo ni mtu na hufunguliwa na mtu.

(d) Kukwepa mawazo hasi.

Mawazo hujenga! "Awazalo mjinga, ndilo litakalomtokea". Ikiwa kama mtu atapokea na kuhifadhi mawazo hasi, ajue anajidumaza. Mawazo chanya huongeza rutuba katika ukuaji wa mtu.
Kwa bahati mbaya, binadamu tumezungukwa na mawazo hasi takribani kila tuishipo. Adui mbaya ni yule anayedhamiria kwa makusudi kumvunja mtu nguvu/ hamasa mtu mwingine.
Undugu huja bila uchaguzi, ila marafii huchagulika. Ikiwa mtu ameambiwa na mtu mmoja 'HUTOFANIKIWA' anahitaji watu kumi na sita kumwambia 'UTAFANIKIWA' ili kumrudishia hari.

(e) Kuheshimu kanuni na masharti.

Kwa watu wenye kazi wanapaswa kufanya kazi wa mujibu wa kanuni, miogozo na sheria za maeneo ya kazi. Kufanya kazi kwa misingi ya kanuni husaidia kupunguza migongano inayopelekea utendaji mbovu. Ni vigumu kufanya kzai kwa mujibu wa sheria, lakini inawezekana kupunguza uwezekano wa migawanyiko na makundi yanayofanya utendaji wa mtu kushuka na hatimaye kuondolewa kazini.

1 comment: