Monday, July 23, 2012

MISINGI YA KUWALINDA WATOTO DHIDI YA MAPENZI YA JINSIA MOJA

Janga la mahusiano ya kimapenzi baina ya watu wa jinsia moja ni changamoto kubwa sana katika malezi ya watoto. Kwa kiasi kikubwa mapenzi ya jinsia moja huchangiwa na sababu za kimazingira na chaguo la mtu husika. Japokuwa, kwa kiasi kidogo, aina hii potofu ya mahusiano inachangiwa na sababu za kibailojia.
Hali ilikuwapo kabla hata ya kuzaliwa Yesu Kristo. Yote kwa ypote, ni lazima kupambana na hali hii na kuishinda. Misingi ifuatayo yafaa kutumiwa na wazazi, walezi na jamii kwa ujumla ili kuwalinda watoto dhidi ya janga la mahusiano ya kimapenzi ya jinsia moja.

1. Kuwalinda watoto dhidi ya unyanyasaji wa kijinsia.

Wazazi na walezi wanapaswa, kwa nguvu zao zote, kuhakikisha usalama wa watoto. Kuwalinda watoto wasitendewe unyama dhidi ya jinsia yao kama kama ulawiti na ubakaji.

Kwa mfano, mtoto wa kike aliyebakwa hujenga chuki dhidi ya wanaume, hivyo hukua na hasira dhidi ya mwanaume yeyote yule hata atakapokuwa mkubwa. Kutokana na chuki dhidi ya wanaume, mtoto huyo huimarisha mahusiano hususani ya kimapenzi dhidi ya wasichana mwingine mwenye chuki dhidi ya wanaume kama alivyo yeye. Lengo la kufanya hivyo ni kutaka kutimiza mahitaji yao ya kimapenzi.

Unyanyasaji mkubwa wa kijinsia hufanyika majumbani; unyanyasaji wa kijinsia hufanywa na watu wanaoheshimika kama baba wa kambo, baba mdogo, mjomba, shangazi, mfadhili n.k. Hivyo, wazazi na walezi wanapaswa kuwa makini sana dhidi ya watu wanaoishi au kuwalea watoto wao.

2. Kuwakuza watoto katika jinsia zote.

Wazazi ndio shule ya kwanza kwa watoto. Watoto hujifunza kutoka kwa wazazi maana na majukumu ya baba na mama (au mme na mke).
Hivyo, baba anapaswa kuwa mfano mzuri wa kuigwa kwa watoto wa kiume, na mama kuwa mfano mzuri wa kigwa kwa mtoto wa kike kupitia maisha yao ya kila siku.

Ikiwa kama ni vigumu kwa mzazi mmoja kushiriki katika malezi, mtoto wa jinsia husika atengewa mazingira yatakayomwezesha kuiga na kuishi kadiri ya jinsia yake. Kwa mfano, kupata nafasi ya kuona jinsi familia za jirani zinavyoishi.

3. Kutomkaripia mtoto vikali kutokana na tabia yake.

Wazazi na walezi wananapaswa kuwa makini pale wanapowaonya watoto wao kwa kuwa wameonyesha tabia au mienendo hatarishi. Kwa mfano, kutompiga vikali mvulana kwa kuwa anajiremba au kuiga sauti za wasichana.
Makaripio makali huwafanya watoto kukubuhu na kujenga kiburi, na hivyo kuamua kuendeleza tabia husika.

Wazazi na walezi wanapaswa kujua ya kwamba watoto, hususani wakati wa balehe au kuvumja ungo, ni watundu sana na hupenda kuiga kila kitu. Hivyo, wazazi na walezi wanapaswa kuwa na upole huku wakiwafundisha madhara ya tabia hatarishi.

4. Kutoa fursa sawa kwa jinsia zote za watoto.

Watoto huwa njiapanda nyingi hususani wakati wa balehe au kuvunja ungo. Baadhi ya watoto huona ya kwamba jinsia tofauti na yao inapata faida sana. Hivyo huanza kuiga mitindo yao ya maisha, mingi ya mitindo hiyo ikiwa ni hatarishi.

Kwa mfano, watoto wa kike huona watoto wa wakipewa uhuru wa kwenda watakapo, kutopangiwa majukumu au kazi nyingi za kifamilia n.k. Hivyo, wasichana hao huiga mienendo ya kiume ili kujiridhisha. Tabia hii ikiachwa huwafanya wasichana hao kujihususisha kimapenzi na wasichana wenzao. Wazazi na walezi wanapaswa kutoa fursa sawa kwa wote ili watoto wote wafurahie jinsia zao tangu awali.

5. Kuwalea watoto kwa misingi ya dini.

Wazazi na walezi wanapaswa kuwalea watoto kwa misingi ya imani zao. Ili kufanikisha hilo, wazazi na walezi wanapaswa kuishi kandiri ya imani zao ya kila siku.
Malezi ya kidini huwafanya watoto kuona muhimu wao kwa mujibu wa jinsia zao.

Kwa mfano, wazazi kuwasimulia watoto habari za watu maarufu waliomtumikia Mungu katika dini husika kwa jinsia. Pia kuwaambia watoto ya kwamba Mungu alimuumba mtu mke na mtu mme ili wamtumikie.

6. Kuwalea watoto kwa mujibu wa jinsia zao.

Mtoto wa kiume anapaswa kulelewa kama mtoto wa kiume ili aweze kuwa mwanaume, na mtoto wa kike vivyo hivyo. Hata kama mtowazazi waliyoipendelea, mtoto aliyezali maadili mema na mwenendo unaokubalika.

Kwa mfano, ikiwa wazazi walipendelea mtoto wa kwanza awe wa kike, na akazaliwa mtoto wa kiume; wanapaswa kumlelea mtoto huyo kama wa kiume, na si kumdekeza. Watoto wengi wa kiume wanaodekezwa huwa mashoga.

Ikiwa kama wazazi na walezi (jamii kwa ujumla) watafanikiwa kuwalea watoto kwa misingi hiyo; kabla ya mtoto kuanza maisha tofauti na ya familia, kwa mfano kwenda shule ya kulala (bodi), changamoto ya mapenzi ya jinsia moja itakuwa imepunguzwa au kumalizika kabisa. Takwimu zinaonyesha kwamba watu wenye mahusiano ya jinsia huimarika wakiwa chini ya umri wa miaka 18.

No comments:

Post a Comment