Monday, August 20, 2012

VIKWAZO DHIDI YA USINGIZI MURUA NA SULUHU ZAKE

Usingizi ni moja kati ya vitu muhmu kwa afya ya binadamu. Kukosa usingizi ipasavyo (masaa 6-8) hupelekea matatizo kama uchovu siku inayofuata, kusinzia siku inayofuata, kupungua uzito, kupungua kinga ya mwili n.k. Kuna imani potofu ya kwamba watoto ndio wanaopaswa tuu kulala muda fasaha.

Kwa kuwa watu wengi hawapo makini katika kuangalia mienendo ya maisha yao, hawawezi kujua sababu zinazopelekea matatizo hayo, hivyo kukosa sululuhu ya kudumu. Zifuatazo ni sababu zinazopekea ukosefu wa usingizi, baada ya kuzijua itakuwa rahisi kwa mtu kukabiliana na changamoto.

Kula chakula kingi muda mchache kabla ya kulala.

Kula chakula kingi, hususani nafaka, muda mfupi kabla ya kulala hufanya mwili utumie nishati nyingi katika kumeng'enya chakula, hivyo kuvuruga utaratibu wa nishati wa mwili. Pia kunywa maji kabla ya kulala humfanya kuamka usiku ili kujisaidia, hivyo kubadili utaratibu wa usingizi.
Mtu anapaswa kula chakula chepesi na maji kidogo angalau nusu saa kabla ya kulala.

Kulala mazingira duni.

Kulala katika mazingira yanayokinzana na utu wa mtu huvuruga utaratibu wa mwili. Mazingira kama; chumba chenye mwanga mkali, chumba chenye joto au baridi kali, kulala kwenye kelele, kulala kwenye godoro laini au gumu sana, chumba kisicho na hewa safi ya kutosha n.k humfanya mtu kukosa usingizi.

Kubadili mfumo wa maisha.

Kubadili mfumo wa maisha na ambao ulikuwa umezoelewa na mwili hutatiza usingizi. Kwa mfano; kumpoteza ndugu au rafiki wa karibu, kuanza kazi mpya, kufanya kazi ngumu, kuingia kwenye ndoa, kuwa na msongo mawazo n.k huwafanya watu wengi kukosa usingizi.
Hali hii huchukua siku chache, ikiwa kama ukosefu wa usingizi itachukua muda mrefu, mtu anapaswa kufanya tahtmini ya kina.

Mazingira duni ya kijamii.

Mazingira duni ya kijamii kama; kulala zaidi ya mtu mmoja kwenye kitanda kimoja, kulala na mtu msumbufu hususani mtoto mdogo, kulala chumba kimoja na mtu anayekoroma, kulala na mtu anayesumbua usiku, kulala chumba chenye wadudu kama chawa, kunguni, viroboto n.k.
Mazingira haya yanasababishwa na umasikini wa kipato.

Matumizi ya madawa.

Kuna aina nyingi sana ya madawa ya hosptalini ambayo, pamoja na kutibu au kupunguza maumivu, hupelekea kukosekana kwa usingizi. Madawa hayo ni kama madawa ya kupunguza maumivu, kupunguza mawazo, madawa ya usingizi n.k.
Mtu anapaswa kusoma maelekezo au kupata ushauri wa daktari kabla ya kutumia dawa yoyote ile ili apate kujua madhara yake na jinsi ya kuyakabili.

Matumizi ya vinywaji baridi na sigara muda mchache kabla ya kulala.

Vinywaji baridi vina kokaini, chai au kahawa ambayo huongeza msukumo wa damu. Matumizi ya vinywaji hivyo kabla ya kulala kukatiza usingizi. Kwa upande wa sigara, ikilinganishwa na watu wasiovuta sigara, watu wanaovuta sigara hukawia kupata usingizi, hivyo, kupata masaa machache ya kulala.
Kuna watu wamezoea kunywa pombe ndipo wapate usingizi, watu hawa ni watumwa wa pombe na wengi wao hutumia pombe kali, baada ya muda, pombe haitoweza kumsabishia usingizi kabiasa au akiwa hana hela ya kununua pombe mtu huyo hatoweza kulala.

Kwa kiasi kikubwa, sababu za ukosefu wa usingizi zipo chini ya uwezo wa binadamu, hivyo, mtu mmoja mmoja na jamii kwa ujumla inapaswa kutengeneza mazingira yanayopekekea usingizi murua, mafanikio ya mtu katika kazi za kujiletea maendeleo, hutegemea, pamoja na mambo mengine, kiasi cha mapumziko anayopata kila siku kupitia usingizi.

No comments:

Post a Comment