Monday, August 13, 2012

MUUNDO WA MPANGO WA MAENDELEO

Watu wengi hushindwa kufikia malengo waliyojiwekea kwa kuwa, moja ya sabau ni, kushindwa kupanga. Kushindwa kupanga hupelekea kushindwa kutekeleza hivyo malengo kutikiwa. Zifuatazo ni hatua muhimu za kumsadia mtu pindi apangapo mradi wa maendeleo.

1. Kununua kitabu cha mipango. Mtu anapaswa kununua kitabu kidogo kwa ajili ya kuratibu na kutunza kumbukumbu za kila siku za mtu binafsi. Vitabu hizi vipo takribani kila duka la vifaa vya shule na ofisini, hujulikana kama "diary" kwa lugha ya Kiingereza.

2. Kuandika mtizamo, lengo au matarajio ya mradi husika. Mtu anapaswa kuandika mradi wake kwenye ukurasa wa kwanza wa kitabu cha mipango. Lengo husika linapaswa kuandikwa kwa herufi kubwa na kwa lugha fasaha. Kwa mfano, LAZIMA NIANZISHE MRADI WA UFUGAJI WA KUKU WA KIENYEJI IFIKAPO MWEZI JANUARI MWAKANI . Mtu anapaswa kuhakikisha anaandika lengo moja tu! Ili iwe rahisi kutekeleza.

3. Kuandika kwa kifupi shughuli muhimu zitakazofanyika na muda mahususi wa kuzifanya ili kufikia lengo kuu. Shughuli hizo hujumuisha malengo madogo madogo. Kwa mfano:

Ni lazima nianzishe mradi wa ufugaji wa kuku wa kienyeji kabla ya mwezi Januari mwakani. Ili kufanya hivyo ninapaswa kufanya yafuatayo; (i) kuomba ushauri kutoka kwa mfugaji maarufu wa kuku wa kienyeji juu ya gharama muhimu wiki ya tatu ya mwezi Agosti (ii) kukamilisha gharama muhimu za kuanza mradi kabla ya wiki ya nne ya mwezi Agosti, kama ikibidi (iii) kuomba ushauri kutoka kwa Afisa Mifugo juu ya aina bora ya kuku, magonjwa n.k wiki ya kwanza ya mwezi Septemba (iv) kufanya utafiti juu ya upatikanaji wa soko la kkienyeji ndani ya wiki ya pili na tatu ya mwezi Septemba (v) kuanza kujenga banda wiki ya tatu ya mwezi Septemba na kukamilisha kabla ya mwisho wa mwezi Oktoba (vi) kununua chakula na dawa muhimu wiki ya kwanza na ya pili ya mwezi Novemba (vii) kununua kuku wa kienyeji; mitetea nane na jogoo mmoja wiki ya kwanza ya mwezi Desemba. Hivyo kuanza ufugaji rasmi kabla ya mwezi Januari.

Mpangilo wa shughuli na muda hutegemea mazigira, uelewa wa mtu, rasilimali akizo nazo n.k. Kwa mfano, kupata mtaji kwa mtu mmoja ikawa changamoto ili hali, kwa mtu mwinine kupata ushauri ikawa changamoto kuu.Mtu apange shughuli rahisi kisha shughuli ngumu baadaye kadiri ya uwezo wake. Ni bora kumshirikisha mtu wa karibu ambaye nimzoefu wakati wa kupanga ili kuepuka kupanga shughuli isiyotekelezeka ndani ya muda fulani.

4. Kurudia kusoma, kufanya marekebosho na kukariri mwongozo ulioandaliwa. Muongozo uwekwe maeneo ambayo ni rahisi kuuona na kuusoma kama kwenye pochi au kwenye mkoba. Hii itaongeza hamasa ya kusoma na kutaka utekelezaji.

5. Kuanza utkelezaji kwa kuandaa ratiba ya hughuli iliyopangwa kufanyika ndani ya muda husika. Katika hatua hii mtu anapaswa kuwa makini sana ili asiruke shughuli aliyoipanga. Ikiwa kama shughuli husika haikuisha ndani ya muda uliopangwa, basi ipelekwe mbele. Kuruka hatua kutasababisha kuvuruga mpango mzima.

6. Kufanya uchambuzi wa hatua kwa hatua. Mtu anapaswa kuangalia utekelezwaji hatua iliyopita ili kufanya marekebisho kwa hatua zitakazofuata kabla mambo hayajawa magumu. Mwenye mradi anapaswa kuwaongoza kwa makini wasaidizi wake wa kila siku.

No comments:

Post a Comment