Monday, November 21, 2011

MALENGO

Malengo ni kama mstari unaotoa mwelekeo (dira) wa mahali anapotaka kufika. Malengo humpa mtu sababu za kujiamini, hususani kama yakitimia.
Kujenga tabia ya kuweka lengo humfanya mtuasonge mbele kuelekea kokote atakako.

Aina Za Malengo.
1) Malengo ya muda mfupi.
Malengo haya ni ya karibu. Huwakilisha mahitaji yanayopaswa kutekelezwa ndani ya muda mfupi, bila hata kutumia nguvu na rasilimali nyingi.
Malengo huchukua kati ya siku moja hadi tisini ili kutimia.

2) Malengo ya kati.
Malengo haya hutegemea malengo ya muda mfupi ili yatimie. Hutegemea nguvu kiasi ili kutimiza malengo ya muda mfupi. Malengo haya huchukua kati ya siku tisini mpaka miaka miwili ili kutimia.

3) Malengo ya muda mrefu.
Malengo haya hutegemea/ huhitaji vitu vingi ikiwamo muda na rasilimali nyinginezo. Huendana na fani ya mtu. Malengo haya huhitaji mikakati na rasilimali nyingi, pia kukamilika kwa malengo ya muda mfupi na wa kati.
Malengo haya huanzia miaka miwili na kuendelea.

Malengo yanaweza kuwa edelevu au pinzani.
Malego endelevu ni yale ambayo hutekelezeka hatua kwa hatua, huanzia na hali aliyo nayo mtu, huchochewa na mafanikio ya kila hatua ya ya mafanikio.
Kwa upande mwingine malengo pinzani ni yale ambayo hutaka mafankip ya ghafla, hukinzana moja kwa moja na hali aliyo nayo mtu.
Kwa ujumla, malengo endelevu hutekelezeka kwa urahisi yakilinganishwa na malengo pinzani
Sifa Sita za Malengo Yanayotekelezeka.
1) Kuandikwa na kushirikisha.
Kila lengo linapaswa liandikwe katika sentensi mbili au tatu. Malengo yaandikwe kwa lugha fupi na fasaha ili mtu aweze kukumbuka mara kwa mara.

Mtu anapaswa kuwashirikisha watu/ mtu ambaye anaelewa na kuamini katika lengo fulani. Mfano mfanyabiashara, mwalimu, daktari n.k. Ushirikishaji hulazimisha uwajibikaji, huleta ushirikiano, pia humsaidia mtu kupata msaada na faragha wakati wa kipindi kigumu.

2) Halisia na kufikika.
Malengo yanapaswa kuwa halisia na yenye kufikika. Ili lengo liwe halisia na lenye kufikika linapswa kuwekwa kwa kuangalia maendeleo aliyofikia mtu na rasilimali (viwezeshaji) alizo nazo mtu kwa wakati anapopanga. Watu wengi kuweka malengo bila kuangalia viwezeshaji kama ushauri, fedha n.k, hali hupelekea utekelezwaji duni wa malengo.

3) Kukubali mabadiliko.
Mtu anapoanza kutekeleza lengo husika, vikwazo na vizuizi huibuka kutoka pasipotegemewa. Lengo linapaswa kukubali mabadiliko pindi hali inapobidi.
Kwa mfano mtu anaweza kubadilisha aina ya biashara ndani ya muda husika kwa sababu kukosa fedha, kupatwa na ugonjwa n.k.

4) Kupimika.
Malengo ni matunda mtu anayoyarajia kupata kutokana na juhudi zake katika uwekezaji. Malengo yanapaswa yawekwe sambamba na vipimo ili kuweza kufuatilia utekelezaji. Vipimo vinapswa kuwa hatua kwa hatua, hii itasaidia kugundua wapi na vipi maboresho yafanwe kuligana na hali husika.

Watu huweka malengo bila vipimo hatimaye madhaifu mazito na yasiyorekebishika huonekena baada ya muda na rasilimali nyingiezo kutumika. Hali hii ianapelaea hasara isiyozuilika.
Kuwa na lengo bila kipimo ni sawa na kutembea njia ndefu inayoelekea mji fulani pasipo kujua ina uerfu gani.

5) kufuatata muda.
Kunapaswa kuwepo muda maalumu katika utekelezwaji wa kila kipengele. Muda hutumika kupima ufanisi. Muda unaopangwa unapaswa uende sambamba na ujuzi, rekodi ya mafanikio ya mpangaji au ya watu anaojifunza kutoka kwao, viwezeshaji n.k

6) Kuwa na lengo mbadala.
Lengo la mtu ni hali anayoitaka mtu baada ya wakati fuani. Kuweka malengo ya ziada (mbadala) hutoa njia mbadala ikiwa hali itakuwa ngumu kiasi kwamba inazuia utekelezwaji ya lengo kuu.

Mfano mtu anapanga kuuza nguo, kama nguo zikidorora afanye biashara ya nafaka. Lengo mbadala linapswa litumie mtaji, maarifa au rasilimali nyinginezo zinazoendana na lengo kuu ili kupunguza gharama na usumbufu wakati wa kubadili.

WATU WENGI HUPANGA KUSHINDWA, NA SI KUSHINDWA KUPANGA.

No comments:

Post a Comment