Monday, November 28, 2011

AZMA KATIKA MAISHA

Azma ni jumla ya mambo yote ambayo mtu anataka maisha yake yawakilishe. Azma ya mtu huendana sambamba na fani (kazi) ya mtu husika.
Ikumbukwe ya kwamba kinachoangaliwa na jamii (watu wengi) si wingi wa miaka aliyinayo mtu au uzoefu bali, ni mchango wake katika maisha ya jamii husika.

Maswali ya msaada (mwongozo) anayopaswa mtu kujiuliza wakati anapoamua azma ya maisha yake katika jamii yoyote ile.
1) Je nataka maisha yangu yaweje?
2) Je naishi maisha sahihi?
3) Je nafanya nini ili kufanikisha maisha sahihi?
4) Je nafanya nini kila siku ili ndoto zangu zitimie?
5) Je nimetoa mchango gani kwa jamii?
6) Je mchango niliotoa kwa jamii ni sawa na jamii ilivyoniwezesha?
7) Je maisha yangu yatajizatiti kwa lipi?
8) N.k

Vigezo Saba Wakati wa Kujenga Azma.

1) Kamilifu.
Mtu anapaswa kutazama vitu kama vitakavyokuwa, na si kama vinavyoonekana.
Kutazama kwa mapana na marefu juu ya kila wazo au lengo alilonalo mtu. Mtu anapaswa kutazama huku akiangalia baadaye, je anachowaza kitafanikiwa?
"Daima tazama juu nawe utakuwa juu"

2) Kuwa na mwanga.
Azma ya mtu lazima itazame mbele, mbele ya ombwe na mbali na upeo wa macho. Mtu anapaswa kujifunza jinsi ya kuitikia, kukumbuka na kukubali "ndoto".
Mwanga huu ni mapokeo ya juu na ya ki-ujasiri. Mtu anayo mamlaka ya kutengeneza taswira kutoka kwenye mawazo aliyonayo kupitia mwanga huu.

3) Kudumu maishani.
Azma ni taswira ya mtu inayowakilisha majukumu ya mtu katika ngazi tofauti-tofauti alizonazo katika jamii. Majukumu aliyinayo mtu yanapaswa kudumu hata kama mwanzilishi hayupo duniani. Sifa hii imewafanya watu wengi wailioondoka duniani kukumbukwa mpaka kesho. Mfano; Martin Luther King Jr, Mwl J K Nyerere n.k

4) Kunufaisha kila mtu.
Azma inayolenga kumnufaisha mtendaji ni ishara ya wazi ya ubinafsi wa hali ya juu, ubinafsi unaotishia usalama na uhai wa jamii.
Azma inapaswa itazame watu wote katika jamii, inufaishe makundi yote ya wanajamii kuanzia; watoto, vijana, wazazi, wazee n.k.
Mfano, je biashara, taaluma n.k yangu ni kwa ajili ya nani?

5) Kushawishi.
Azma inapaswa wakati wote ishawishi imani na uwezo wa mtungaji. Inapaswa imshawishi mtu kufanya kila jitihada zilizo halali lili kutimiza azma husika.
Mfano, kama mtu anataka kuwa mfugaji wa kuku, azma ya kufuga kuku imshawishi atafute msaada kutoka kwa wafugaji, wataalamu wa mifugo n.k ili kufuga kuku kwa ufanisi na si kwa mazoea.

6) Kuchoma.
Azma ya mtu iwe kama moto, moto unaochochewa na imani ya kufanikiwa. Imani ya kufanikiwa huwa kama moto unaoamsha hisia na uwezo wa akili pamoja na misuli kana kwamba, mtu anakuwa na ujasiri na uthubutu juu ya vikwazo vyote vya kibinadamu.

7) Kuwa na manufaa.
Azma ya mtu inapswa kutimiza matakwa ya jamii na dunia kwa ujumla. Iwe na uwezo wa kukabili na ktoa suluhu dhidi ya changamoto zinazomkabili binadamu kwa wakati husika.
Azma inayolenga kuondoa adha kwa jamii hupata msaada kutoka sehemu mbalimbali duniani. Mfano, je azma yangu ya kufungua mradi wa kilimo itapunguza tatizo la ukosefu wa ajira katika jamii yangu?

No comments:

Post a Comment