Monday, November 14, 2011

KUWA NA FURAHA LEO UFAIDIKE LEO!

Leo ni siku ya siku ya kuacha kuishi kwa kutegemea kesho. Kwani leo ni siku ambayo hautaishuhudia tena katika maisha yako, hivyo unapaswa kuifurahia hata kama ni chungu kama shubiri au mwarobaini.

Watu wengi huairisha furaha zao wakisubiri malengo yao yatimie ndipo wafurahie. Baadhi ya watu husema watakuwa na furaha ikiwa tu:
¤ watapata kazi nzuri,
¤ watakapopata wapenzi wa maisha,
¤ watoto wao watakapokuwa wakubwa,
¤ watakapohitimu masomo,
¤ watakapostaafu kazi za ofisini,
¤ n.k.
Watu hutoa sababu nyingi kama hizo zinazowapelekea kuishi kwa huzuni, huzuni wasiyostahili.

Kwa kawaida lengo moja linapofanikiwa ghafla malengo mengine huibuka hivyo, kumfanya mtu kuishi akisubiri furaha maisha yake yote. Inafaa kupambana ili kuwa na maisha mazuri huku akifurahia kila hatua ya mafanikio anayopiga kuelekea hayo "maisha bora"

Mtu anapaswa kujua ya kwamba wakati alionao (siku, saa na dakika) hataushuhudia tena katika maisha yake, ikipita imepita.
Yaliyotokea kabla ya leo na yatakayotokea kesho ni vitu vilivyo nje ya akili ya mtu. Hali halisi ni ile mtu anayoishuhudia wakati husika, wakati ambao anawezakfanya jitihada ili kuleta mabadiliko katika maisha.
Jiulize kama usipokuwa na furaha leo je utakuwa nayo lini?

Kuna njia rahisi ya kumfanya mtu afurahie (siyo aridhike) na hali aliyonayo mayo ni KUJITAMBUA.
Mtu anapaswa kutambua hali ya uchumi yake, jamii yake na yale yote anayoshuhudia ikiwamo changamoto. Kuangalia mazingira yanayomzunguka, kusikiliza kwa makini sauti ya moyo wake na kila kinachoingia akilini mwake.

Kutambua pale mtu alipo hufungua akili na furaha huchukua nafasi ya huzuni. Huzuni inayoletwa na mtizamo hasi kuhusu jana na kesho. Kujitambua huleta hisia chanya na kuonyeha viwezeshaji, viwezeshaji ambavyo husaidia kufanikisha malengo kwa haraka.

Ingawaje mtu hana uwezo wa kuzuia ukweli wa yale anayoshuhudia lakini, anao uwezo wa kumiliki anachoshuhudia ili kimsaidie. Mtu anapaswa kuita furaha na ikaja haraka hata asivyotarajia.

Kwa mfano, kama ntu anajikuta anawaza juu ya upungufu wa kiungo/viungo katika mwili wake, asitishe mawazo hayo na aanze kuamini mambo yatakuwa sawa ikiwa tu atapenda kwani, yeye si wa kwanza na wala hatakuwa wa mwisho. Wapo wengi, watu wengi wenye mapungufu makubwa lakini wamefanikiwa na kuwa watu muhimu katika jamii zao.

Kuna uhusiano mkubwa sana kati ya uwazaji wa mtu na homa. Mwili huathiriwa hasi na mfadhaiko wa akili. Maumivu yoyote ya nwili ni taarifa ya kwamba kuna kasoro na inahitaji suluhu.

Homa huibuka kwa sababu ya kupuuzia taarifa za mara kwa mara zinazotolewa na akili kuptia mwili. Hali inapokuwa mbaya ndipo mtu huchukua hatua za kubadili anavyowaza na kuanza kutibu maumivu.

Mtu anapaswa kuwa makini sana kwa kile mwili unachomwambia, pia kufahamu ya kuwa mwili na akili hufanya kazi pamoja. Akili ndio inayochukua hatamu za kuongoza mwili, ndiyo maana mtu akiwaza visivyo hupata homa ghafla.

Kama mtu atakuwa na mawazo chanya, anayotiba ya uhakika dhidi ya huzuni na homa. Tiba zote hutegemea hisia na mtazamo wa mtu (furaha) ndipo zitoe matokea ya haraka. Mtu anavyohisi juu ya jambo fulani, mfumo wa neva hutoa ishara zinazoathiri mfumo wa kinga ya mwili.
Kumbuka njia (kinga) bora katika kuzuia homa au kupunguza makali ya homa hata kama mtu anatumia dawa ni kuiamuru akili iite furaha.

No comments:

Post a Comment