Monday, November 7, 2011

UPWEKE

Mtu mwenye upweke hukumbwa na hisia za woga, woga ambao unazorotesha hali ya afya. Mara zote woga hujikita kwenye mahusiano ya mtu binafsi, mahusiano ya mtu na mtu/jamii, kazi, uchumi, afya na mustakabali kwa ujumla.

katika hatua za awali upweke unaweza ukamkumba mtu bila ya watu wengine kufahamu. Upweke na msongo wa mawazo ndio vikwazo vikuu kwa afya ya akili.
Kwa bahati mbaya hali ya maisha ya nyakati hizi huchangia kwa kiasi kikubwa tatizo la upweke pia hukuza ukubwa wa tatizo.

Jinsi ya Kuzuia Upweke.

Dalili za upweke hazionekani kirahisi, huonekana wakati tatizo limekua kubwa. Njia zifuatazo zinafaa ili kuepusha hali ya upweke.

1) Kuzungumza juu ya changamoto.
Kuzungumza na mtu sahihi ni hatua muhimu sana katika kutatua changamoto. Inafaa kumtafuta mtu wa karibu na ambaye anao uzoefu juu ya changamoto husika.

Watu wanaoishi peke yao (wenye kujitenga na marafiki, jamaa n.k) wapo katika hali mbaya zaidi, inafaa mtu kuwa na mahusiano mazuri na wale wanaomzunguka. Mawasiliano mazuri hufanikisha mazungumzo juu ya changamoto na huakikisha suluhu sahhihi inapatikana.

2) Mapumziko.
Kukosa au kuwa na mapumziko hafifu hukaribisha upweke, hivyo mtu anapaswa kupanga na kutumia muda hata kama ni kidogo kupumzisha mwili na akili.

Kuna njia nyingi za kufanya mapumziko kama; kutembelea wagonjwa, kwenda maeneo ya mbali, kufanya kazi za bustani, kuogelea n.k. Inategemea na muda mtu alionao, gharama, mapendekezo yake n.k

3) Kupumua.
Zoezi la kupumua ni rahisi na lenye mafanikio ndani ya muda mfupi. Kupumua hutumika kuondoa chembe za uchovu na upweke katika mazingira yoyote yale.

Zoezi lenyewe ni, kuvuta pumzi ndani taratibu huku tumbo (na si kifua) limetanuliwa, kisha kutoa hewa taratibu, zoezi lirudiwe mara tatu au nne mfululizo na mara mbili au tatu kwa siku, kadiri ya mapenzi ya mtu.

4) Kula sahihi.
Tafiti zimeonyesha ya kwamba kufungua kinywa kwa protini huondoa mawazo yanayofanana na upweke. Kufungua kinywa kwa protini kukifuatiwa na wanga, matunda n.k. Pia maji ya wastani wa glasi nane (inategemea na mazingira na aina ya vyakula) kwa siku.

5) Kujjihusisha na kikundi.
Inapaswa mtu kuwa katika aina yoyote ya kikundi, hususani kikundi kinachotoa mwamko, kikundi cha wakulima, wakina mama wajasiriamali,
n.k.
Katika kundi mtu anapata uzoufu kutoka kwa watu mbalimbali jinsi ya kupambana na changamoto za kimaisha. Hii inajenga ujasiri dhidi woga wowote ule.

6) Kutafuta habari kuhusu changamoto.
Mtu anapaswa kutafuta habari kutoka vyazo tofauti pindi anapohisi mambo hayaendi sawa. Kuna ushauri mwingi na wenye kufaa kwenye vitabu, majarida, CD/DVD n.k.

Habari sahihi huondoa wasiwasi kuhusu changamoto za kiafya, kikazi n.k. Kwa mfano mtu anaweza kupata ukweli juu ya vidonda vya tumbo, shinikizo la damu, kisukari n.k kwenye mtandao wa intaneti.

7) Kujiamuru.
Kujisemea maneno ya kutia moyo kama "hakuna kitakachotokea", naelekea kushinda", "Mungu wangu nipe amani, "Mungu uniodolee woga n.k kwa sauti na mahali tulivu.

8) Kuzuia mawazo.
Mtu anapaswa kuzuia mawazo yanayoleta woga au yanayoendana na woga. Mfano, mtu kuhisi anaugonjwa usio na tiba n.k. Mawazo kama hayo yanaonekana mapema, hivyo ni rahisi kuyazuia kwa kuyakataa.

9) Kuukabili woga.
Mtu anapaswa kumudu mbinu za kumpa ujasiri pale anapokumbana na hali tata na yenye kutisha. Hali aliyonayo mtu hutegemea jinsi anavyowaza hususani wakati wa changamoto, kukifuatiwa na uumbaji wa picha na baadaye upweke huota mizizi.

JIPIME
Jibu "N" kama jibu lako ni NDIO na "H" kama jibu lako ni HAPANA.
1) Je mapigo yako ya moyo yanaridhisha?
2) Je kama mtu akitaka kukukopa unashindwa kujibu "hapana"?
3) Je unapata jazba kwa mambo yasiyo na faida?
4) Je ni vigumu kusema "hapana" kwa muuzaji"
5) Je huwa unapata hofu bila sababu za msingi?
6) Je unaogopa sana na hali hiyo inakuuzunisha?
7) Je rafiki akikukosea unaweza kumwambia alivyofanya siyo sahihi?
8) Je unakataa au kuahirisha mikutano/mialiko?
9) Je mara zote unahisi kutoridhika?
10) Je unaweza kuhoji au kudai haki/stahili yako?
11) Je kama hujafikia muafaka na mpinzani wako unakaa kimya?
12) Je ni mzito kufanya maamuzi?
13) Je hutaki kupokea sifa?
14) Je mara nyingi unakuwa na hofu?
15) Je una uthubutu?
16) Je unaweza kuendelea na mazungungumzo na mtu baada ya kutofautiana?
17) Je unahisi kutoweza kutatua matatizo yako?
18) Je kama mtu akikupa upendeleo, unaweza kuukataa?
19) Je mara nyingi unafanya kazi kwa shinikizo?
20) Je kama hujaelewa kitu unaweza kuuliza hadharani?

UFAFANUZI WA MAJIBU.
¤ kama "N" ni kati ya 0 - 7, hauko kwenye hatari ya upweke.
¤ Kama "N" ni kati ya 8 - 12, upo kwenye hatari na unapswa kuchukua hatua (za hapo juu) ili kuweka mambo sawa.
¤ Kama "N" zaidi ya 12, ni mpweke, unapaswa kuchukua hatua na pia kumwona mwanasaikolojia kwa msaada zaidi.

No comments:

Post a Comment