Monday, October 10, 2011

SIRI RAHISI INAYOWASHINDA WENGI

Je, unayotabia ya kuandika malengo na kuyafanyia kazi? Kujiwekea malengo ndio mbinu kuu na sahihi ya kufikia mafanikio yoyote yale! Mbinu hii hutumika katika katika mipango yote, ya muda mfupi na muda mrefu. Kuandika matarajio ni kama kuchora ramani ya njia kuelekea kule mtu anakotaka kufika.

Kuandika malego kumewafanya watu wa kawaida kuwa watu mmarufu na muhimu katika jamii, vivyo hivyo kutoandika matarajio kumeshusha vipawa vya watu wenye uwezo.
Watu wengi wanajua ya kwamba kuandika malengo yao ni hatua muhimu kuelekea kwenye mafanikio yoyote yale lakini hawafanyi hivyo.

Kazi ngumu na yenye manufaa ni "kuamua". Inahitajika nguvu kidogo kufamya mambo makubwa lakini inahitajika nguvu kubwa kuamua mambo makubwa. Kufanya maamuzi ni kazi ngumu na inaathiri maisha ya watu wote. Kuwa mtu sahihi hutegemea maamuzi sahihi.

Mtu anahitaji zana sahihi ili kufikia malengo. Zana hizo ni KALAMU na KARATASI. Watu wako tayari kutembea umbali mrefu ili kukwepa kazi ya kuandika, wanaweza kuwaza, kuongea n.k lakini hawako tayari kuandika.

Hii ni kwa sababu kuandika kunahitaji kuwaza kwa kina. Kama huamini, jaribu kuanika chochote ndani ya sekunde kadhaa bila ya ya kufikiri.

Kuandika kuna nguvu mara kumi zaidi ya kuongea. Kuandika kunaanmsha seli za ubongo zilizolala na kumlazimisha mtu afikiri kwa kina na kwa ufasaha.

Kama mtu hajandika malengo yake, basi afahamu ya kwamba hayuko makini (serious). Kuwaza bila kuandika hufutika baada ya dakika chache lakini kuwaza na kundika hakufutiki kamwe!

Kitendo cha kuandika unayotaka ni kama kuwasha sakiti ya umeme kunavyopelekea taa kuwaka, mashine kufanya kazi n.k. Nusu ya tatizo litakuwa limepatiwa ufumbuzi kama mtu ataandika mbinu anazoamini ndio sahihi na jinsi ya kuzitekeleza.

Kuandika huleta nguvu ya ajabu inayoondoa woga, inayoleta matumaini na ujasiri. Kuandika malengo kunamfanya mtu kuchukua hatua ili kuyafikia, hubadilisha mtizamo na muonekano wa mtu husika.

Kuandika malengo kunagharimu dakika chache, huokoa zaidi ya miaka ishirini ya kuwa na matrajio (ndoto).
Kuona malengo yaliyoandikwa kwenye karatasi kunagonga kengele inayomtaka na kumlazimisha mtu kufanya jambo lolote ili kufikia lengo/malengo.

Mtu anatakiwa kujiwekea lengo/ malengo machache ili iwe rahisi kuyafanyia kazi mfano; "nataka kuwa mwandishi", "nataka kuwa mfanyabiashara" au "nataka kuwa mkulima" n.k.
Lengo /malengo hayo yaandikwe na kuwekwa sehemu tofauti-tofauti ambazo ni rahisi mtu husika kuona na kusoma mfano; kitandani, mezani, jikoni, mfukoni n.k.

Kisha lengo/malengo yasomwe kila siku asubuhi na jioni (kabla na baada ya kulala), huku mtu husika akiwaza kufanya jambo lolote siku inayofuata ili kufikia lengo.
Mtu anahitaji kukumbushwa zaidi kuliko kufunzwa.

Mbinu nyingine zinazohusiana na kuandika malengo ni:
-kujiambia kwa sauti katika maeneo tulivu "nitafanikiwa"
-kuangalia mafanikio ya watu waliokuwa na lengo/malengo sawa
-kusoma machapisho ya watu waliofanikiwa mara kwa mara
-kuongea na watu sahihi na wenye malengo sawa
-kusoma machapisho juu ya lengo lako
-kusikiliza mihadhara, radio, CD n.k
kujihusisha na watu wenye mafanikio.

No comments:

Post a Comment