Wednesday, October 19, 2011

TASWIRA BINAFSI

Taswira binafsi ni jinsi mtu anavyojifafanua mbele za watu. Ni picha ya mtu binafsi anayoionyesha mbele ya watu wengine. (mimi ni nani?).
Taswira binafsi inampa mtu uwezo wa ktoa, kupokea na kukabiliana na changamoto za kimaisha.

Taswira binafsi inayojengwa kwenye misingi ya woga, wasiwasi, kutokujiamini n.k huonyeshwa kwa hisia hasi.
Taswira binafsi iliyojengwa kwenye misingi ya upendo, heshima, imani, uelewa n.k huonyeshwa kwa hisia chanya.

Vitu Vinavyoathiri Taswira Binafsi

Kuna viti vitatu vikuu vianavyoathiri taswira binafsi ya mtu.
1) Mawazo na hisia wakati wa utoto.
Katika miaka saba ya kwanza, watoto hujenga mfumo wa kuthaminisha na ambao huongoza maisha yao yote.

Watoto hupenda na kutafuta mafundisho mazuri, mawazo mazuri, hisia nzuri na mienendo chanya.
Kwa bahati mbaya, hawana kinga dhidi ya mawazo mabaya, mafunzo mabaya na mienendo hasi.
Kwa kutokuwa na uwezo wa kuzia maovu, mawazo na matendo ovu huwatawala na kudumaza ukuaji wa taswira binafsi iliyo bora.

2) Mazingira
Mazingira yana mchango mkubwa sana, kwani ndio chanzo cha uthibitisho wa yote mtu aliyojifunza utotoni.
Mtu anapokuwa katika mazingira fulani kwa muda mrefu huchukua/ kufanana na tabia za mazingira husika.

Kamataswira ya mtu inakinzana na mazingira husika, kuna machaguo matatu:
¤ kubadilisha mazingira
¤ kubadilisha taswira binafsi
¤ kuondoka katika mazingira.

3) Makundi.
Makundi huleta ufanano. Makundi chanya husaidia kukuza taswira binafsi kwa; kuchambua mambo kwa kina, kukuza uelewa, maana n.k
Makundi hasi hudumaza taswira binafsi ya mtu kwa; kuzuia kutafuta habari, kuzuia kufikiri, kusistiza "haiwezekani" n.k.

Tabia Tano za Watu Wenye Taswira Binafsi Iliyo Duni.

Watu wenye ufinyu wa taswira binafsi ni wengi, kwa bahati mbaya zaidi wengi wao ni vijana.
Watu hawa wana/huonyesha sifa zifuatazo.

1) Kukwepa majukumu.
Watu hawa hukwepa kuchukua majukumu yao, hukwepa wajibu au matokeo ya yale waliyoyafanya.
Kwa mfano, mvulana anaposababisha ujauzito na kuamua kumsaliti msichana husika.

Kama mtu asipochukua majukumu yake, kamwe hawezi kubadili hali aliyonayo hata kama anaichukia sana. Mfano, mtu hawezi kupata mafanikio ikiwa ataacha kufanya kazi kwa bidii na kubaki kuilaumu serikali tu.

2) Kukimbia changamoto.
Mtu anapokumbana na changamoto, kuna machaguo matatu; kupambana, kusahau, na kukimbia.
Mtu mwenye ufinyu wa taswira huamua kukimbia changamoto husika. Mfano, kijana anapoamua kukimbia nyumbani baada ya kutofautiana na wazai/ walezi.

Mtu ataimarika kama tu! Atakabiliana na changamoto husika. Kukubali na kukabili changamoto huleta ujasiri na imani na kumwezesha mtu kukabliana na changamoto nyingi zaidi.
Je mtu atakimbia chanagamoto ngapi ili afanikiwe?

3) Kukosoa muada wote.
Watu wenye upumgufu wa taswira hutafuta mtu/watu wa kukosoa pindi makosa yanapotokea.
Watu hawa hukosoa kila kitu bila hata kuonyesha chembe ya kujenga, uungwana, heshima n.k.

Kukosoa kwa chuki hubomoa sio tu mkosolwe bali hata mkosoaji.
Kukosoa kunakojenga huambatana na upendo, heshima, utu n.k. Husaidia kujenga na kuimarisha watu wenye mapungufu. Huwafanya watu (mkosoaji na mkosolewaji) wakubalike katika jamii husika.

4) Husubiri watu watoe suluhu ya changamoto.
Watu wenye taswira binafsi duni hukaa na kusubiri rafiki, ndugu n.k watoe suluhu ya changamoto zinazowakabili. Kwa mfano, kijana anasubiri wazazi wamtafutie kazi.

Kama mtu atasubiri watu wampatie majibu ya changamoto zinazomkabili, mtu huyo kamwe hawezi kukua na kuimarika kwani kufanikiwa au kutaofanikiwa kunamuimarisha mtu.

5) Kupuuzia mambo.
Watu hawa huishi kana kwamba kila kitu ni sawa (OK!). Hujisahaulisha changamoto zinzowakabili. Huona hakuna haja ya kuwaza mbinu mbadala ili kuboresha hali husika. Huamini kila kitu ni sawa na inatosha, hakuna haja ya kuumiza kichwa zaidi.

Mfano, mtu anagundua amekosea moja ya hatua katika kufanya kitu fulani, kisha anajisemea haina tatizo, hata fulani alikoesea n.k. Hachukui hatua ili kurekebisha hatua husika hata kama anao uwezo wa kufanya hivyo.

No comments:

Post a Comment