Monday, October 24, 2011

NJIA 12 ZA KUKUZA TASWIRA BINAFSI

Ili kukuza na kuimarisha taswira binafsi, inampasa mtu kutumia njia zifuatazo wakati wote wa maisha yake hata kama atapata mafanikio mapema.

1) Kuwa mwaminifu.
Yapasa mtu kuwa mwaminifu, uaminifu unaoanzia moyoni. Yapasa kuweka nadhiri ya uaminifu kati ya nafsi ya mtu na yale ayatakayo (malengo).

Hii itamfanya mtu kuwa makini wakati wote anapohusiana na jamii inayomzunguka, vitendea kazi, na mazingira husika.
Ili kuona ukuu na umuhimu wa kutofanya makosa ya kizembe.

2) Kujenga taswira.
Taswira ni ramani au picha ya yale mtu ayatakayo, ni hatua ya kwanza katika uumbaji.
Taswira ya matarajio inaweza kujengwa kwa kusoma, kujihusisha na watu wanaoona vyema mbele na ambao wanaoweza kukuza ufahamu.

3) Kupumzika.
Kupumzika ndio moja ya njia sahihi ya kupunguza/ kuondoa msongo mawazo.
Mtu anaweza kupumzika kwa kwenda mazingira taofauti na yale aliyoyazoea, kuomgea na watoto wadogo n.k

Msongo mawazo hupunguza nishati na kinga ya mwili na kupelekea ugonjwa. Ugonjwa unashusha / unapunguza makadirio ya mafanikio.

4) Kuwa na imani ya ushindi.
Imani a ushindi ni hisia kali anayokuwa nayo mtu juu ya kukamilisha kitu fulani na kuona matunda yake.

Imani ya ushindi huonyeshwa na jinsi mtu anavyoongea, anavyotenda na anavyoishi.
Imani ya ushindi huvuta hisia za watu, watu huwa tayri kutoa msaada wa hali na mali ili kufanikisha malengo ya mtu husika.

5) Kujenga tabia njema.
Tabia na mienendo hukua na kuimarika baada ya muda mrefu, baada ya urudiaji wa mara kwa mara kwa mara.
Tabia jema ni zle zinazopelekea: afya njema, mapumziko sahihi, mlo kamili, mazoezi ya mwili na uwazaji sahihi.
Mtu hujenga tabia, tabia humjenga mtu.

6) Kuamua kuwa na furaha.
Kuwa na matarajio mazuri kila siku, kutarajia kila siku kuwa ya furaha huamuliwa pindi mtu anapoamka na kutaka kufanya kila kitu kwa amani.

Kudhamiria mema na mazuri wakati wote. Kama mtu atdhamiria kila siku kuwa njema, basi mtu huyo hujenga usumaku na mema aliyoyatarajia.

7) Kujivua gamba.
Gamba ni hali inayomjenga na kumlinda mtu dhidi ya watu wengine.
Lengo lake ni kuficha hali halisi ya mtu husika.
Ni kama uigizaji kana kwamba mtu anavaa husika usio wake. Mfano masikini kutumia pesa kidogo alizopata na watu matajiri na maarufu ili kuficha umasikini.

8) Kuwa na hisani.
Lazima kutambua hali halisi, matatizo na mahitaji ya wengine, na kuwa tayari kutoa msaada.
Mtu anapaswa kusaidia wenzake ambao hawajafanikiwa baada ya kupita hatua kulani ya mafanikio.
Kufanya hivyo humweka mtu karibu na Muumba na huinua utu wa mtoaji na mpokeaji.

9) Kuimarika kutokana na makosa.
Makosa ni masomo kimaisha kwa wenye busara.
Mtu anapaswa kujifunza kupitia makosa ya wengine (ili asianguke walikoanguka wanzake) na sio kufanikiwa kwao.

Pia kujifunza kupitia makosa aliyoyafanya mtu kwa uchambuzi wa kina ili kupata sababu za kukosa.
Kutumia makosa (yako na ya wengine) kama njia kuelekea mafanikio.

10) Kukubali udhaifu.
Kama mtu hatakubali udhaifu alionao kamwe hawezi kuushinda. Mtu asipokubali madhaifu yake hawezi kujua chanzo chake na hawezi kuchukua hatua za makusudi ili kuweka mambo sawa. Kutokubali kushindwa lili kujipanga zaidi hukuza ukubwa wa tatizo.

11) Kujikubali.
Kama mtu hatajikubali/ kuikubali hali yake au mtu atajifananisha na watu wengine, basi mtu huyo hutaka kujitenga na hali yake, nguvu zake na hisia zake.
Mtu ambaye hujikataa (hujisaliti) hawez kujua yeye ni nani na ana thamani gani.

12) Kuendelea kukua.
Maisha ni mchakato wa kupitia furaha, huzuni, magumu, changamoto n.k
Mtu anapaswa kukua kwa kpitia uelewa wa kina na uthubutu wa kufanya maamuzi, hasa maamuzi magumu (maamuzi yanayoamua mustakabali wenye heri) wakati wa changamoto.

No comments:

Post a Comment