Monday, October 31, 2011

NYAKATI KATIKA MAISHA

Mtu anapaswa kufahamu ya kwamba katika kukua kwake lazima apitie nyakati/ hatua tofauti. Ili kufahamu hilo mambo manne yanahitajika kueleweka kwa kina, mambo hayo ni yafuatayo.
Maisha ni bustani.
Maisha ni bustani ambayo ina maua mazuri (muelekeo chanya). Kama mtunza bustani (mtu husika) asipofanya jitihada kuondoa magugu (mawazo hasi) maguugu hayo huua maua.

2) Kila tendo lina matokeo.
Katika maisha kama mtu asipokuza kipawa alichopewa na Mungu vyema na kama mtu asipochukua hatua za makusudi kipawa chake kitatoweka.

Kwa kila analowaza na kutenda mtu lina madhara (ya kukuza au kudidimiza ) kipaji chake. Kama mtu akikaa kimya, ulimwengu humchagulia na daima humchaguila mabaya

3) Kila kitu kina wakati.
Maisha yana nyakati/ hatua, nyakati/ hatua ziko katika mtiririko. Nyakati zinadumu kwa kipindi cha miaka 20 -25. Kama mtu atashindwa kumudu changamoto za wakati haua fulani, mtu huyo atakuwa na kipindi mgumu sana mbeleni.

4) kuna kani mbili katika ulimwengu.
Takribani vitu vyote vinavyotokea katika maisha hutegemea nguvu za binadamu. Kila anchofanya binadamu huzaa wema au ubaya. Wema au ubaya ndio matokeo ya kazi za binadamu.

Hatua Anazopita Binadamu Katika Maisha

1)
Wakati wa elimu
Hii ni hatua ya kwanza, hatua hii huanza mwaka 0 mpaka 20 - 25. Katika hatua hii binadamu hujifunza misingi na kanuni muhimu za maisha. Mtu hujifunza kwa kusoma, kuandika, kuhesabu, kufikiri na kufanya maamuzi.

Mtu hujenga taswira binafsi, kujiamini, imani, woga, ujasirii n.k. Mtu hupata elimu/ ufahamu kutoka kwa wazazi/ walezi, waalimu, au mtu yeyote aliye karibu.
Kama hatua hii itajengwa kwenye misingi imara ya ukweli, uungwana, nidhamu, upendo, n.k hakuna kitakachomshinda mtu maishani.

2)
Hatua ya hisia na mihemko.
Hatua hii ya pili huanza miaka 20 - 25 mpaka miaka 40 - 50. Katika hatua hii mtu huanza kukumbana na changamoto za maisha, channgamoto za utu uzima kama mapenzi, vilevi, kazi n.k. Watu wengi huangusha/ kushindwa na hatua hii. Katika hatua hii tabia zinaweza kumjenga au kumbomoa mtu.

Wanaume huangushwa na hisia zinazoletwa na ulevi, mapenzi, kutaka kutawala n.k. Ili hali wanawake huangushwa na hisia zinazoletwa na kutaka kupata utulivu wa kimapenzi (kupendwa)

Ili kumudu hatua hii mtu anapaswa kujenga programu ya kipato, programu ambayo itamhakikishia mapato hayazidi matumizi. Mipango yote ya pesa ibajetiwe, kuwe na fungu la matumizi ya kawaida na la uzalishaji (uwekezaji au kukuza kipato). Mtu atumie fursa zinzotolewa na makampuni kama kununua hisa, biashara ya mtandao, kununua fedha za kigeni n.k ili kumhakikishia kipato siku za baadaye.

3)Hatua ya kuwa na nguvu.
Hatua hii ya tatu huanzia miaka 40 - 50 mpaka 60 - 65. Katika hatua hii mtu hufikia hatua ya hali ya juu ya mafanikio au kushindwa.
Mtu huonyesha kumudu au kutomudu mbinu za kufanikiwa.

Changamoto kubwa katika hatua hii ni kuchagua kuwa mwema au mbaya. Watu hulazimika kurudia masoma ambayo hawakuyamudu katika hatua za nyuma. Hupata changamoto ya kukabiliana na misukosuko ya kimaisha ambayo inahitaji nguvu nyingi na suluhu la haraka.

4)
Hatua mgando.
Hatua hii huanza mika 60 - 70 mpaka 100 na kuendelea. Mtu huchanganua alichofanya na kuvuna katika kuishi kwake, hutafuta mbinu za kufanya matunda ya kazi zake yadumu milele hata milele.

Mtu hutaka kuona kazi za mikono yake hazifi na ndoto zake zinadumu daima. Hali hiyo husisimua nguvu za nafsi, mwili na akili kwa kiwango cha juu. Mtu haogopi wala kutishwa na changamoto zinazomkabili na yuko tayari kufa akipigania anachotaka.

MIAKA ILIYOTUMIKA NI YA WASTANI KWA WATU WALIO WENGI, KWA BAADHI YA WATU BAADHI YA HATUA HUCHUKUA MIAKA MICHACHE SANA LAKINI WATU WOTE HUPITIA HATUA ZOTE.

No comments:

Post a Comment